WASANII TUSIWE WATU KULAUMIWA KILA WAKATI! BALI KUSHAURIWA,

WASANII LAZIMA WAANGALIE KWA MAKINI MIKATABA NA MUDA KUTUMBUIZA

Baada ya vyombo vya habari kuandikia kwa wingi tukio la fujo zilizotokea wikiendi ya 30.Augost 2014 katika show ya mwanamuziki Diamond, Blog ya jamii na timu ya Michuzi Media  imefanya juhudi za kutaka kusikia maoni na mtazamo wa mwanamuziki wa Tanzania aliyeupigania muziki wa Tanzania katika soko la ughaibuni kwa miaka 21 si mwingine bali ni Kamanda ras Makunja wa FFU
au Ngoma Africa Band.

Michuzi media ilianza kwa swali ?: Ras Makunja nini mtazamo wako  kwa
Yaliyotokea Stuttgart.?

Kamanda Ras Makunja: " Kwanza nianze kwa kuwapa pole wale wote waliopatwa  na usumbufu na maumivu yawe ya mwili,hisia au hali kutokana na tukio lile,kwa kweli tuliposikia tulistuka sana sana" ,Ras Makunja alisema.

Kwa kuwa sisi sote tunajua ugumu wa msanii anapokuwa On Tour hususan ugenini ,kuna taarifa za awali ambazo msanii ni vigumu sana kuzipata,taarifa ambazo ,pengine zinaweza kumsaidia msanii kwa namna moja au nyingine,kwa kweli msanii anapokuwa ugenini ni sawa na usiku wa kiza.Ras Makunja alisisitiza

Tunacho shukuru Mungu pamoja na yote yaliyotokea pale hatukusikia kama kuna mtu aliyepoteza uhai,maana uhai ni zawadi ya Mola kwa viumbe wake.

Wito wangu kwa wadau na washabiki kwa kuwa nyinyi ndio ma-boss zetu,na sisi wasanii au wanamuziki ni watumishi wenu,ningewaomba msichoke kuunga mkono mara mnaposikia msanii au mwanamuziki,au bendi inapiga sehemu fulani,Kwa sababu Chereko Chereko na mwenye mwana.

Fujo zilizotokea pale Stuttgart kila moja kasoma katika vyombo vya habari na nyinyi ndio mahakimu,lakini mimi si msemaji wa upande wowote pale bali kama msanii ningeomba msimuhukumu msanii kwa kosa la mtu mwingine.

MICHUZI MEDIA : Unawashauri nini wanamuziki  wenzako kutoka nyumbani  wanaokuja   kutumbuiza ?

Ras Makunja: Ushauri wangu nimeshausema mara nyingi katika vyombo vya habari kuwa, Wasanii wa nyumbani lazima wanapopata mikataba waipeleke kwa mameneja na mwanasheria ili isomwe na kueleweka kipengele kimoja baada ya kimoja mfano: taratibu za malipo cash au? na muda wa kulipwa kabla au baada ya show: Hotel,Bima ,VAT,Ulinzi na Kingine muhimu ambacho mara nyingi  ndicho chanzo cha mizozo ni malipo na muda wa kutumbuiza hili lazima liwe wazi tena ndani ya mkataba,Mfano show inaanza saa 4 usiku hadi 7.usiku basi lilwe wazi.

Unajua kuna baadhi ya mapromota wanapenda sana kutufanya wasanii kuwa mashine, mara nyingi wanavunja utaratibu "anakuweka hoteli na yeye anasubiri watu wajae ukumbini au wanunue vinywaji kwanza ,sasa 
watu wakishalewa unategemea nini? ni fujo tu lakini kama mkataba unaeleza time ya kutumbuiza na mwisho wa show,ata kama kuna watu wawili msanii anatumbuiza.

"WASANII WA AFRIKA MASHARIKI WAPENDWA SANA ULAYA"
Ras Makunja alisema baada miaka 21 ya kupigania soko na moyo wa wadau na washabiki wa sanaa za Afrika Mashariki sasa sanaa zetu zimeshika soko na baadhi ya wasiopenda maendeleo wanatutazama kwa macho ya makengeza ! 

Wasanii lazima tuangalie sana sana nani wa kufanya nae kazi,katika music Industry kuna baadhi ya watu wanamfanya msanii ni kipande cha ndimu "anakamua na kutupa ganda" 

Msanii anapata tabu kujenga jina kwa miaka,eti promota anataka kulibomoa kwa dakika usipokubaliana na yake,lazima wasanii wajichunge sana.

Wasanii wa Afrika Mashariki tunawapa wakati mgumu wapinzani wetu,na wapinzani wetu wanajua vema kuwa pia sisi ni wakarimu hapo ndipo wanapojaribu kutumaliza na ukarimu wetu.

Nawashauri wasanii wezangu wale wanaokuja ujerumani,kabla hujasafiri jaribu kuwasiliana na umoja wa waTanzania Ujerumani(UTU) email yao hii kamati.utu@googlemail.com ili upate information muhimu,hakuna
atakaye kuingilia katika biashara au mkataba wako lakini ushauri ni muhimu.

Pia lazima tujijue kuwa kwa sasa tunatishia soko na tayali lipo mikononi mwetu kwa maana hii wapinzani wanajaribu kujifanya wao ndio mapromota lazima tujipange na kutambua nani wa kufanya nae kazi na kwa makubaliano yepi.

Habari za uhakika tunazo kuwa mwaka 2015 wasanii wa Afrika Mashariki ndio wanaotakiwa kwa wingi hapa ughaibuni,tumieni nafasi hiyo.

KARIBUNI SANA KATIKA SOKO LA UGHAIBUNI NA MKIPATA NAFASI ZA
KUTUMBUIZA LAZIMA MKAMUE BILA YA HURUMA.
Asanteni, pia nawashukuru sana Michuzi Media kwa kunipa nafasi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Rasi ushauri wako nimuhimu sana kuzingatiwa. kwa uzoefu wangu,ni hivi tatizo hili alitaisha kwa hizi shoo za uchochoroni za kuwapigia watanzania wakenya na waganda ,nk. kama shoo anazo fanya RAS ZA MATAMASHA YA KUELEWEka sidhani usumbufu kama huu unaweza kutokea.mimi huwa najiuliza kaukumbi kama hako unavyokaona ni promota anaganga njaa tu wapelekeni wasanii wetu kwenye matamasha makubwa ambayo hata mikataba yake ni ya kueleweka. pia sio kama nawasema vibaya wanageria ila chunga sana unapo fanya nao kazi mimi niko huku hawa jamamaa na wengine west afarika nikuwa makini nao . tujifunze wasanii wa bongo, muda sasa umefika kutafuta matamasha makubwa. kaka s

    ReplyDelete
  2. kamanda mkuu ras makunja asante sana
    kwa ushauri wako kwa hawa vijana wetu wanamuziki chipukizi,kwa weli inasikitisha sana wanapopata nafasi ya kuja ughaibuni lakini wanakuwa wapo gizani bila ya kuwa na information muhimu,wajaribu kuwasiiana na jumuiya za wa TZ za huko.Kamanda asante sana kwa ushauri

    ReplyDelete
  3. kamanda mkuu wa ffu,ushauri wako mzuri umeelemika lakini hawa vijana wenu ni wabishi hawapendi kumshirikisha mtu mtaalam katika shughuli ndio maana yanawakuta mengi
    usisahau usemi ule wa makaidi afaidi mpaka siku ya Idd

    ReplyDelete
  4. Makunja mbona nyie mpo ndani ya gemu kwa miaka na mnatumbuiza maelfu ya washabiki hatujawai kusikia mmechelewa jukwaani,katika sakata la
    Diamond lazima kulikuwa kuna ubabaishaji fulani

    ReplyDelete
  5. Promota Britts Event inasemekana ndio zake kila show anayoandaa mwisho wake ni timbwili

    ReplyDelete
  6. Ras makunja mkuu wa himaya ya viumbe ajabu Anunnaki tunashukuru kwa somo,lakini watoto wenu wa kizazi kipya hawana nidhamu wala utaratibu
    wanapoitwa sehem wao pesa mbele uhai baadaye,sasa katika sakata lile labda watasoma

    ReplyDelete
  7. Bwana kamanda mkuu tumekusikia sisi wadau kila wakati tupo pamoja nanyi wasanii ,tungependa nanyi basi muwe mnawaeleza hao waandaaji wenu kuwa
    TIME MORE THAN MONEY wakati ni uhai,
    tusiwe tunawasubiri kama vie tuna msubiri YESU

    ReplyDelete
  8. kamanda mbona nyie mkienda kwenye show zenu mnawekewa ulinzi mkali! sasa kwa nini Stuttgart pasiwe na ulinzi mambo yamepelekwa kienyeji enyeji

    ReplyDelete
  9. mkuu makunja mimi nakubaliana nawe
    ukarimu wa wabongo unawapa upenyo wapinzani wetu ,nina wasi wasi labda katika makubaliano ya Diamond na promota mpopo kulikuwa na ukarimu wa kuitana ndugu au brother matokea yake ndio vile

    ReplyDelete
  10. kaka makunja ata ukiwashauri vipi? watoto wenu wa bongo flava ni wabishi wameweka sifa mbele kuliko uhai wao,angalia sasa wanijeria wanavyo waweka kinyumba

    ReplyDelete
  11. wasanii wa bongo kweli wababaikaji,
    mmekuwa limbukeni wa ajabu angalia mnaijeria anababaikiwa na ndiye mnamwita promota ni ujinga

    ReplyDelete
  12. Kaka Makunja wewe haukuwepo pale,
    mimi nimesafiri na mume wangu na marafiki zangu kutoka wurzburg mpaka Stuttgart kwa ajili ya kuungamkono
    tulichoambulia rafiki yangu kapigwa chupa ya mkono,mume wangu kapoteza pochi ni aibu,siendi tena kama muandaaji ni yule mjinga mpopo.
    Mdau
    Judith Otieno

    ReplyDelete
  13. ujinga tena ni ujinga yaani tulipoteza muda na pesa zetu pale kwa ajili ya kwenda kununua bia mpaka 4.00am please never again

    ReplyDelete
  14. Joka kuu kamanda ras makunja mtawala wa himaya ya viumbe wa Anunnaki,tumekuelewa lakini mbona nanyi wasanii wa bongo hambadili tabia zenu ? kila kukichwa ni uhuni tu sasa sisi wadau tutawapa shavu vipi? kwa miradi hii ya kutiana hasara

    ReplyDelete
  15. Makunja unajua kinachouma zaidi ni kuona nyinyi wasanii badala kwenda mbele sasa mnashirikiana na watu wanao warudisha nyuma,sasa nani ? mchawi wa kazi zenu kama siyo nyinyi wenyewe! badilikeni

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...