Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la mfuko wa pensheni la PPF mjini Mwanza jana jioni.Wengine katika picha kutoka kushoto,ni Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli, Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana Wiliam Erio, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Adam Malima, Mwenyekiti wa Bodi ya PPF Bwana Ramadhani Kija, na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evaristi Ndikilo.
Jengo la Kitega uchumi la mfuko wa pensheni wa PPF lililozinduliwa rasmi na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mjini Mwanza jana jioni.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio wakiangalia madhari nzuri ya jiji la Mwanza wakiwa katika jengo jipya la kitega uchumi la mfuko wa pensheni wa PPF muda mfupi baada ya kulizindua mjini Mwanza jana jioni.
Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya PPF Bwana Ramadhani Kija(watatu kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio(kulia) wakimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua jengo la kitega uchumi la PPF mjini Mwanza jana jioni.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio akitoa maelezo kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ndani ya mgahawa uliopo katika jengo jipya la kitega uchumi la PPF muda mfupi baada ya kulizindua rasmi mjini Mwanza.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na viongozi na wafanyakazi wa Shirika la PPF baada ya kuwa amezindua Jengo la Kitega Uchumi la Shirika hilo katikati ya Jiji la Mwanza jana, Ijumaa, Oktoba 10, 2014. Rais Kikwete yuko katika ziara ya siku tatu ya kikazi Mkoani Mwanza.(picha na Freddy Maro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ujenzi wa majengo mazuri unaonyesha tunapiga hatua nzuri za maendeleo za kuboresha miji yetu tuendelee kuwekeza nchini kote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...