JACKLINE MASANJA A.K.A JACK WA NJIAPANDA ENZI ZA UHAI WAKE.
Ilikua ni miaka kumi iliyopita (10) mwaka 2004, nikiwa ndio kwanza nimeanza kufanya kazi chini ya kaka yangu Dr Sebastian Ndege na chini ya uangalizi wa karibu sana wa boss Ruge Mutahaba na Boss Joseph Kussaga nilipokutana na wewe mdogo wangu Jackline Masanja kupitia Njiapanda ulipokuwa unatafuta msaada ukiwa mgonjwa sana. 

Nakumbuka Dr Sebastian Ndege alipokuona tu alikubaliana na mimi kuwa tuache kila mpango tuliokua nao tuweke nguvu zote kwako. Kweli ulikua unaonekana ni mgonjwa, Kwa kutumia nafasi ya Dr Ndege kipindi hiko akiwa ndio anakaribia kumaliza masomo yake ya udaktari na mimi ndio kwanza nikiwa mwaka wa pili wa udaktari tulifanikiwa kuhakikisha kuwa unapata matibabu ya haraka uliyokua unayahitaji sana. 

Ulikua shujaa sana kukubali kusema kuwa uko tayari Dr Ndege atangaze hali yako mbele ya uma wa WaTanzania na kwa ruhusa yako tukafanya kipindi na wewe huku ukiwa mgonjwa na ukasema kuwa umeathirika na kwa kipindi kile kinga yako ilikua chini sana (CD4 zilikua 4). 

Wewe ulikua ni watu wa mwanzo kabisa kuja mbele ya umma kuongea kuhusu hali halisi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI na maradhi ya UKIMWI. Tulikuita shujaa na Muhimbili ulipokua unatibiwa kipindi kile wahudumu wote walikuita Jackie wa Njiapanda (ndio chanzo cha kumuita jina hilo miaka yote hii). Kutokana na juhudi nyingi zilizofanyika ulipona kabisa na ukarudi kwenye hali yako ya kawaida ya kawaida na ukaendelea na maisha yako.

Kutokana na yote yaliyotokea mimi na Dr Ndege tukaona ni vyema kama tutakuomba ukae na sisi kama Njiapanda na uendelee kutusaidia kwa kuwa Njiapanda ilikua imekua sana na waliokua wanahitaji msaada walikuwa wanaongezeka kila kukicha. Hukusita kukubali na kuanzia miaka hiyo ukawa unatusaidia kushughulika na wote wanaohitaji msaada wa Njiapanda. Ni wengi uliwachukua na kukaa nao kwako ingawa hali yako ya kiuchumi haikua nzuri sana kusema eti wewe ni tajiri.

Miaka ilienda na ukaendelea kupambana na maisha huku ukiendelea vyema. Nakumbuka vizuri sana sakata la dawa ya Babu wa Loliondo lilipoanza mimi na wewe tulikua hasi na chanya. Mimi nilikua napinga sana kwa kuwa nilikua na sababu za kisayansi na wewe siku zote ulikua unakasirika kwa kuwa ulikua ukiamini kuwa dawa inaponya. Ukaniomba nikuruhusu uende na kweli tukakubaliana tukafanya mchakato na ukaenda. Tukakubaliana kuwa mimi nachohitaji ni kimoja tu nacho ni kukutumia wewe kama somo kwa hiyo tukarekodi kila kitu kabla hujaenda kwa babu na tukafanya kipindi maalum. 

Ukasema kinga yako ni ngapi na kila kitu wala hukuogopa. Ukaenda Loliondo ukanyweshwa kikombe na ukarudi. Tukafanya kipindi ukasema unaendelea vizuri. Tukaendelea na vipimo na maisha yakaenda. Miezi miwili baadae nakumbuka nilikua nimekaa kliniki nikakuona kwa chini unatembea huku unajikongoja, nikakufuata pamoja na manesi wa pale clinic tukakuchukua tukaendelea na uchunguzi tukagundua kuwa kinga yako imeshuka sana kwa kuwa baada ya kwenda kwa babu hukuendelea na dawa (kinga ilikua 14). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. DU JAMANI BINTI HUYU. NIMESIKITIKA TANA KUZIKIA JINSI ALIVYOUWAWA. NILIKUWA MPENZI SANA WA KIPINDI HICHO CHA NJIA PANDA WAKATI ULE NA YEYE ALIKUWA AKISHIRIKI. JAMANI BINADAMU MBONA TUMEKUWA NA ROHO YA KINYAMA NAMNA HIYO. YAANI MTU UNATHUBUTU KUUTOA UHAI WA BINADAMU MWENZIO UTADHANI WEWE UTAISHI MILELE. REST IN PIECE JACK.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...