Mmoja kati ya maafisa wa polisi kikosi cha usalama barabarani Tabora mjini akimuonesha mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila kifaa maalumu kinachotumika kupima kiwango cha ulevi kwa madereva wazembe.

Kikosi cha zimamoto mkoa wa Tabora kikionesha vifaa vinavyotumika wakati wa uokoaji ajali zinapojitokeza.
Sherehe za wiki ya usalama barabarani mkoa wa Tabora zilianza kwa maandamano yaliyopita mitaa mbalimbali hadi viwanja vya mazoezi ya Jeshi la Polisi Tabora ambapo wananchi walishiriki maandamano hayo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora kikosi cha usalama barabarani SSP Peter Mnyandwa akitoa taarifa ya ongezeko la  ajali za barabarani mkoani Tabora ambapo zaidi ya watu 150 wamefariki dunia katika ajali 399 huku watu 520 wamejeruhiwa katika ajali 185.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akihutubia katika sherehe hizo za wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambapo mbali ya kusikitishwa na taarifa ya ajali hizo lakini alisema kuwa asilimia 75 ya ajali hizo zinatokana na makosa ya kibinadamu na hivyo kuzitaka mamlaka husika kuchukua hatua ya kudhibiti kupunguza ajali hizo ikiwa ni pamoja na kutotoa leseni kwa madereva ambao hawajapata mafunzo ya udereva darasani.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...