1
WaziriMkuu, MizengoPinda akisalimiana na Mbunifu wa kimataifa wa Mavazi, Sheria Ngowi alipotembelewa jana nyumbani kwake Masaki jijini Dar esSalaam. (Picha Zote: AtuzaNkurlu-SheriaNgowi Brand).
2
Mbunifu wa kimataifa wa Mavazi, Sheria Ngowi akimuonesha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baadhi ya vitambaa vya kisasa vya suti ambavyo vitatuka Kumtengenezea Waziri Mkuu jana jijini Dar es Salaam.
3
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiangalia na kuchagua aina ya vitambaa vya suti amabvyo vitatumika kutengenza baadhi ya Suti Zake alipotembelewa na Mbunifu wa Kimataifa wa Mavazi, Sheria Ngowi jana jijini Dar es Salaam.(Picha Zote: Atuza Nkurlu-Sheria Ngowi Brand).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Tuwaunge mkono madesigner waki Tanzania.

    ReplyDelete
  2. Ankal, nimeguswa sana na taarifa hii. Mheshimiwa Pinda ameonyesha mfano mzuri kwa kumtambua na kumtumia mbunifu wa mavazi m-Tanzania, wakati wengine wanaenda kununua ughaibuni.

    Tunao wataalam wananchi katika fani mbali mbali, kuanzia ubunifu wa mavazi, kama hivyo, hadi upishi, kama tunavyoshuhudia kwa Chef Issa ambaye ni mshindi wa kimataifa. Watu wenye wadhifa katika jamii wakiwa na tabia ya kuwaenzi hao wananchi kama anavyofanya Mheshimiwa Pinda, manufaa yake ni makubwa. Itatusaidia kujenga utamaduni tofauti na huu ulioota mizizi wa kushabikia mambo ya ughaibuni, na itasaidia kuboresha uchumi wetu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...