Mwandishi wetu,Arusha

WIZARA ya Fedha, imeitaka Bodi ya Wataalam wa Ugavi na Manunuzi nchni (PSPTB), kutafuta ufumbuzi wa tatizo la kufanya manunuzi bila kuzingatia thamani halisi ya fedha na kuwataka waajiri kuacha mara moja kuwaajiri watu wasio na sifa kufanya kazi hizo

Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano wa tano wa mwaka wa Siku mbili unaofanyika kwenye jengo la Mikutano la AICC jijini Arusha ambapo aliwataka Wataalamu hao kuzingatia maadili na miiko ya kazi yao.

Amesema katika bajeti ya mwaka 2014/15 serikali imetega bajeti ya Sh trilioni 20 kati ya hizo asilimia 65 hadi za 70 zinatumika kwenye manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali,hivyo taaluma hiyo kuwa na umuhimu wa kipee katika kudhibiti mapato ya serikali yasitumike vibaya.

Awali Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Sr. Dk. Hellen Bandiho, amesema kauli mbiu ya mkutano huo “Thamani halisi ya fedha za Manunuzi” ikilenga kuhakikisha serikali inapata huduma bora kulingana na fedha inazotumia ili kuinua uchumi wa nchi.

Amesema Bodi hiyo imezalisha wataalam zaidi ya 23,000 katika ngazi mbalimbali ambayo ni sawa na asilimia 47 pekee huku waajiri wengi wakiwa wamewajiri watumishi wasiosajiliwa na Bodi hiyo.
Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima akiongoza na maafisa wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) katika mkutano wa Siku mbili unaofanyika kwenye kituo cha mikutano cha AICC, jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Kwani hawa mawaziri wa fedha wapo wangapi mala mwiguru nchemba mala adam malima

    ReplyDelete
  2. Mchangiaji wa kwanza habari inasema naibu waziri wa fedha siyo waziri wa fedha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...