Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) Bw. Charles Chacha akiongea
na waandishi wa habari kuhusu hali ya usalama wa anga Tanzania na namna
Tanzania ilivyofanikiwa kupunguza idadi ya ajali za ndege.
Katibu Mkuu
wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaaban Mwinjaka akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa
habari leo jijini Dar es salaam kuhusu maadhimisho ya miaka 70 ya Usafiri wa
anga duniani yanayoendelea nchini na namna Serikali kupitia Mamlaka ya Anga
Tanzania (TCAA) ilivyojipanga kuhakikisha usalama wa ndege na abiria wanaotumia
anga la Tanzania.
Afisa mwongoza
ndege wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Bi. Mossy Kitangita akiwahamasisha baadhi ya vijana
na wanafunzi waliotembelea banda la maonesho la kitengo cha kuongozea ndege (hawapo
pichani) kusoma masomo ya Sayansi ili waweze kupata fursa ya kujiunga na fani ya
uongozaji wa ndege ndani na nje ya nchi.
Afisa mwongoza
ndege wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Bi. Mossy Kitangita (kulia) akimweleza Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaaban Mwinjaka namna kitengo cha uongozaji wa ndege katika
uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kinavyofanya kazi na changamoto
wanazokabiliana nazo.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...