Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika kikao na watendaji wa kampuni ya DermCappello yenye Ubia kati ya Watanzania na Waitalia waliofika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini ili kueleza nia yao ya kuzalisha umeme wa jua na kujenga kiwanda cha kutengeneza vifaa vya umeme jua. Kutoka kushoto ni watendaji wa kampuni ya DermCapello, Eng. Steven Chaula, Capello Giuseppe na Giuseppe Capello. Kulia ni Mchumi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Nicolaus Moshi, Mwanasheria wa Wizara, Abbas Kisuju, na Eng. Innocent Luoga, kamishna Msaidizi Nishati anayeshughulikia Umeme.
Rais wa kampuni ya Capello ya Italia, Capello Giuseppe akizungumza wakati wakati wa kikao kati ya kampuni hiyo na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini. Kampuni hiyo iliyoungana na watanzania na kuunda kampuni ya DermCapello walifika Wizara ya Nishati na Madini ili kueleza nia yao kuwekeza katika umeme wa jua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Muwongo yupo kwa sana waliopiga kelele bungeni nadhani hawamfahamu JK subiri uone

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...