Naibu kamishina wa Bima Tanzania, Juma Makame (katikati) akishuhudiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Jubilee Insurance, George Alande (kushoto) na Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa wakati akisaini nyaraka za makubaliano ya huduma ya BimaAFYA kati ya Vodacom Tanzania na Jubilee Insurance itakayotolewa kupitia huduma ya M PESA, ambapo Watanzania wenye kipato cha chini watajiunga na huduma hiyo na kupata matibabu kwenye hospitali zaidi ya 150 nchini. Ili kujiunga na huduma hiyo mteja anatakiwa kupiga namba *150*57#. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa huduma ya BimaAFYA kati ya Vodacom Tanzania na Jubilee Insurance itakayotolewa kupitia huduma ya M PESA, ambapo watanzania wenye kipato cha chini watajiunga na huduma hiyo na kupata matibabu kwenye hospitali zaidi ya 150 nchini. Ili kujiunga na huduma hiyo mteja anatakiwa kupiga namba *150*57#. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Jubilee Insurance, George Alande na Naibu Kamishina wa Bima Tanzania, Juma Makame. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...