Umoja wa klabu za michezo za maveterani Dar es salaam,  chini ya uratibu wa klabu za Singasinga na Tazara,  unatangaza rasmi kwamba  shughuli ya kurehemu wanachama wenzetu ambao wametangulia mbele ya haki itafanyika JUMATATU 12/1/2015, ikiwa pia ni  sehemu ya kuadhimisha sikukuu ya Mapinduzi.

Ratiba itaanza  Saa 7 mchana katika viwanja vya Leaders club jijini Dar es salaam. Dua zitafanyika  kutoka kwa Father Oscar na Sheikh Kipoozeo. Dua hizo zitafuatiwa na Chakula cha pamoja cha mchana kitachoandaliwa na Mpishi maarufu nchini, Chef  Saidi Bajia,  na  baadae burudani mbalimbali za  nguvu zitaendelea. 

Karibuni tujumuike wote... 

Pichani chini ni shughuli kama hii zilizofanyika miaka iliyopita.
- Imetolewa na Balozi Cisco Mtiro, Mratibu mkuu wa shughuli hii.
wanachama wa klabu za michezo za maveterani Dar es salaam wakiwa katika shughuli hiyo ya kuwakumbuka wenzao miaka ya nyuma
Mapochopocho
wadau
Kila mtoto wa mujini alikuwepo
Vilaji

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Thanks very much Ambassador Cisco. Great important event. Please do list the names as much as you can. Last time I went through the list, I had a shock of my life to hear Saad S of TAZARA passed away.

    Ahsante and thanks for organising this again and all the best.

    Mdau - Australasia

    ReplyDelete
  2. muombeni miola wetu mlezi awarehemu wote waliotangulia halafu kuleni chakula mkimaliza mtawanyike msianze kupiga mambo yetu yale (mvinyo)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...