Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wananchi wa Sikonge mkoani Tabora wakati alipopita kukagua barabara za mkoa huo. Dkt. Magufuli aliwaahidi wananchi hao wa Sikonge kuwa Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mpanda-Tabora kupitia Sikonge yenye zaidi ya kilomita 359 itakayofadhili na Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wananchi wa Sikonge mara baada ya kuwahutubia.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ludovick Mwananzila kushoto akizungumza na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli kabla ya kuhutubia mkutano kwa wananchi wa Tabora. Waziri Magufuli aliwaeleza wananchi kuwa Wizara ya Ujenzi itawasimamia kikamilifu Wakandarasi wanaojenga barabara katika mkoa huo na kuhakikisha miradi yote inakwisha kwa wakati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...