Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya kulia akimkabidhi Katibu Tawala Wilaya ya Kalambo Bi. Mapinduzi Severian Katiba pendekezwa leo tarehe 14 Februari 2015 kwa niaba ya wananchi wa Wilaya hiyo ambao watapata fursa ya kuiona na kuisoma kwa ajili ya kuipigia kura ya maoni mwezi Aprili mwaka huu.


Sehemu ya washiriki wa hafla hiyo, Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kalambo muda mfupi baada ya kukabidhi Katiba pendekezwa. Aliwataka wananchi hao kujitokeza kwa wingi mwezi April kwa ajili ya kuipigia kura katiba hiyo na kutopotoshwa kwa namna yeyote ile na watu wasioitakia mema nchi yao. Alisema kuwa katiba hiyo ni nzuri kwani imegusa maslahi ya watanzania wote na ustawi wa taifa kwa ujumla.

Baadhi ya wananchi wakionekana kujifunika na mwanvuli kufuatia mvua iliyokua ikinyesha mwishoni mwa hafla hiyo.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...