Na Mwandishi Wetu

Mpango wa Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) Jumanne, Machi 10, 2015 unaadhimisha miaka 12 ya kuleta mageuzi ya utawala na utungaji wa sera bora barani Afrika.

Maadhimisho hayo yatafanyika kwa namna na staili mbalimbali Barani Afrika katika nchi wananchama wa Mpango huo ikiwemo Tanzania.

Hapa nchini kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mtendaji wa APRM, Mpango huo utaadhimisha siku hiyo kwa kufanya mjadala wa wazi kwenye Chuo Cha Diplomasia kilichopo Kurasini, Dar es Salaam utakaohudhuriwa na viongozi mbalimbali na wanadiplomasia.

Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni "Kuwawezesha Wanawake ili kuwa na Afrika yenye Amani na Fanaka". Kauli Mbiu hii inatoa fursa ya kuangazia mchango wa Wanawake katika ujenzi wa Tanzania iliyo bora zaidi, changamoto za usawa wa kijinsia na maoni ya nini kifanyike.

“Lazima sote tuendelee kupinga ukatili kwa binadamu wenzetu; ikiwa ni pamoja na ukatili wa kijinsia na  ukatili kwa watu wenye Albinism; na kuangalia njia za kuimarisha ushiriki wa Wanawake katika masuala ya Utawala bora, kuleta Amani na Maendeleo ya jamii kwa ajili ya Ustawi wa raia wote,” alisema Rehema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...