Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa wamachinga Tanzania SHIUMA,pamoja na viongozi wa UVCCM kata za jiji la Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa nyumbani kwake Ngarash Monduli mwishoni mwa wiki mara baada ya kumkabidhi mchango wa shilingi milioni moja ili achukue fomu kuwania urais kupitia CCM.Pia walimkabidhi Ngao na mkuki atakavyotumia katika safari yake ya matumaini.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akionesha kitambulisho cha uanachama wa shirikisho la Umoja wa wamachinga Tanzania (SHIUMA) baada ya kukabidhiwa na uongozi wa shirikisho hilo mwishoni mwa wiki huko Monduli.Pia alikabidhiwa shilingi milioni moja na ombi la kumtaka achukue fomu kuwania urais kupitia CCM.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akihesabu Fedha kiasi cha Shilingi Milioni 1, alizopewa na Shirika la Umoja wa Wamachinga Tanzania pamoja na Umoja wa Vijana wa CCM  (UVCCM) kata za jiji la Mwanza ili achukue fomu kuwania urais.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hapa mnatoa taarifa kama hizi zenye mlengo wa kampeni tukitoa maoni yetu sio wenye mtazamo tofauti hamyatoi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...