Kontena la Lori hilo likiwa limewekwa pembeni baada ya kuondolewa kwenye eneo la Ajali.
Picha na mdau Baraka wa Chibiriti
Picha na mdau Baraka wa Chibiriti
Watu zaidi ya 30 wanasadikiwa kupoteza na maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya sana katika ajali mbaya iliyotokea mapema leo asubuhi,maeneo ya Changarawe,Mafinga Mkoani Iringa,iliyohusisha Lori la Mizigo na Basi la abiria la Kampuni ya Majinja lililokuwa likitokea Mkoani Mbeya kuelekea jijini Dar es salaam.
Ajali hiyo imetokea baada ya Lori hilo la Mizigo lililokuwa likitokea Jijini Dar kuelekea Mbeya kuligonga na kuliangukia basi hilo wakati lililokuwa likikwepa shimo kubwa lililopo katikati ya barabara wakati wakiwa kwenye mwendo walipokuwa wakipishana.
Hali ya Uokoaji wa maiti na majeruhi walionasa kwenye ajali hiyo bado ni tete na hasa kutokana na ukosefu wa Gesi ya kukata basi hilo kukosekana eneo lote la Mafinga,Juhudi zinafanyika ili kuweza kuokoa majeruhi pamoja na maiti.
Globu ya Jamii inaendelea kufuatilia kwa ukaribu tukio hili ambalo ni la kusikitisha sana na ni msiba mkubwa kwa taifa,na tutaendelea kujuzana kupitia hapa hapa.
Mungu azipokee na kuzilaza mahala pema peponi roho za marehemu wote katika ajali hii na awajaalie kupona kwa haraka majeruhi wote - Amin.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI
RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mheshimiwa Amina Masenza
kufuatia ajali mbaya ya barabarani iliyotokea tarehe 11 Machi, 2015 Mafinga katika
Mkoa wa Iringa katika eneo lijulikanalo kwa jina la Changarawe, ambayo imepoteza
uhai wa watu zaidi ya 40 waliokuwa wakisafiri kwa basi hilo na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Ajali hiyo
imetokea baada ya basi la Kampuni ya Majinja Express walilokuwa wakisafiria
watu hao kutoka Mbeya kwenda Dar es Salaam
kugongana na lori lililokuwa likitokea Dar es Salaam
kwenda Mbeya, hivyo kusababisha kontena lililokuwa limebebwa na lori hilo kuliangukia basi.
“Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa
sana kufuatia taarifa za vifo vya watu zaidi ya 40 huku wengine kadhaa wakijeruhiwa
katika ajali hii mbaya ambayo imesababisha simanzi na majonzi makubwa kwa
familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu”, amesema Rais Kikwete akiomboleza msiba
huu.
“Huu ni msiba
mkubwa, na Taifa kwa ujumla limepata pigo kubwa, hivyo naomba
upokee salamu zangu za rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kutokana na ajali
hii iliyotokea Mkoani kwako. Naomba, kupitia kwako, rambirambi zangu na pole nyingi ziwafikie watu wote waliopotelewa
ghafla na wapendwa wao. Namuomba
Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema azipokee na kuzilaza Roho za Marehemu wote
mahala pema peponi, Amina”, ameongeza kusema Rais Kikwete.
Katika Salamu
zake hizo, Rais Kikwete amewahakikishia wafiwa wote kuwa yuko pamoja nao katika
kuomboleza msiba wa ndugu na jamaa zao, lakini amesema, pamoja na machungu yote
ya kupotelewa na ndugu na jamaa zao, anawaomba wafiwa wawe na moyo wa uvumilivu
na subira wakati huu wanapoomboleza vifo vya wapendwa wao.
Aidha, Rais
Kikwete amehitimisha rambirambi zake kwa
kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema watu wote waliojeruhiwa
kwenye ajali hiyo wapone haraka, ili waweze kuungana tena na ndugu na jamaa
zao.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
– Dar es Salaam .
11 Machi, 2015
Poleni wote mliofiwa na wale walioumia katika ajali hii mbaya.
ReplyDeleteHivi tanroads kwa nini hawazibi haya mashimo
ReplyDeleteJuzi nami nusu nigongwe na roli njia ya dodoma baada tu ya kibaigwa kama unaenda dom wakati lilipokuwa linakwepa shimo
Tanroafs mashimo yanatumaliza jamani
Ni UZEMBE mkubwa wa TANROADS wanaacha vijishimo barabara kuu mpaka yanakuwa makubwa na kusababisha ajali mbaya kama hizi, tungekuwa na utaratibu wa kuwajibishana mambo haya yasingetokea.
ReplyDeleteAudhubillah
ReplyDeleteMichuzi, sisi huku wakati wote twapenda kujua habari zinazotokea nyumbani, na ni blog yako ndiyo inayotusaidia. But often we are on the move and use ipads or iphones. So mheshimiwa, why dont you ask wakina Manywele na jamaa hapo mitamboni kucreate apps for the blog
ibrahim
Mungu azipokee roho zote za marehemu waliofariki katika ajali hii mbaya. Madereva kuweni waangalifu barabarani munasababisha ajali nyingi zinazoweza kuepukika. Na hilo shimo lililosababisha ajali ya watu wengi hivyo, jamani lilishindwa kufukiwa hata kwa halimashauri ya Iringa mpaka kusababisha kutoa roho za watu wengi hivyo? hii ndo Tanzania. Wapumzike kwa amani na majeruhi wapone haraka.
ReplyDeleteKwa kweli nimekerwa sana na huu uzembe wa hii sehemu ya barabara ya Mafinga..eneo la Changarawe na ajali ambayo ingeweza kuepukika. Mashimo makubwa yamekuwepo muda mrefu..sana kweli wakala ka wa barabara (TANROADS-ngazi ya mkoa) wameshindwa kufukuia haya mashimo..jamani kwani ni ghali sana kuweka kifusi..changarawe na kupasawazisha..mimi ni mdau natumia sana barabara hii inauma sana mara nyingi tunasema uzembe wa madereva lakini hili lingeweza kuzuiwa mapema
ReplyDeleteMungu atunusuru na hizi ajari mungu wapokee waliopoteza maisha na uwaponye kwa haraka majeruhi wote
ReplyDeleteBarabara zote za TZ zina nashimo ya ghafla na wakati mwngine wanachimba wakati wana repair na kuacha hivyo kwa siku kadhaa. Mfano Mafinga mpaka Njombe yapo kibao. Mbezi mpaka Chalinze ndiyo usisikie. Roho mkoboni. Lakini cha kushangaza mabasi na malori yanapita huko kwenye mashimo kwa kasi ya ajabu. Polisi na viPaso vyao wanasubiri rushwa kwenye sehemu za 50mph. Aibu hii kwa taifa lenye neema za kila aina.
ReplyDeleteTumechoka na maneno ya rambirambi kinachotakiwa ni vitendo. Barabara hiyo ni kuu, ilipaswa ijengwe njia nne kuepusha ajali jamani. Hivi lini Tanzania itasikia kilio cha watu. Au mpaka mtu aliyekufa aje kutoka kuzimuni aseme sasa ajali basi? no no Inatosha kama wadau wanaopinga mauaji ya albino. Inatosha ajali Tanzania tumechoka sana sana.
ReplyDelete
ReplyDeleteMAAMUZI SAHIHI YA MADEREVA NDO SULUHISHO LA KUPUNGUZA AJALI, NA KUNUSURU MAISHA YA WATANZANIA. VYANZO VYA AJALI NI VITATU
1.DEREVA
2.GARI YENYEWE NA
3. BARABARA
LAKINI DEREVA ANAPEWA ASILIMIA 72 ZA KUSABABISHA AJALI.
Hii Serikali yetu basi tu..Pesa za kununua magari ya luxuries, kwenda kutembelea nchi za nje kwa trip ambazo hazina tija zipo nyingi tu..lakini pesa za kufukia mashimo..TANROADS wanasema hakuna...jamani..
ReplyDeleteUzembe wa madereva pia unachangia kama huyo Dereva wa basi anapita eneo hilo kila siku na anajua lina mashimo makubwa kwanini hakuchukua tahadhari ya kupunguza mwendo tumechoshwa na ajali hizi za kizembe ambazo zingeweza kuepukika mwenyezi mungu azilaze pema peponi roho za marehemu wote waliopoteza maisha katika ajali hii mbaya.
ReplyDeleteAmen
Maneno hayavunji mfumpa. Vinatakiwa vitendo. Ndugu wafrica wenzangu tutumie akili na marifa. Tuachane na ujinga uliotujaa kutatua matatizo yetu. Jambo ili la ajali linakost maisha ya mamilioni ya watanzania. Muda wa kutumia maneno bila vitendo umeshapitwa na wakati. Vyanzo vya matatizo vinajulikana, lakini atujali, tunawaza peana pole tu basi yamekwisha. Ndani ya mwezi tena yale yale. Hivi Lini? Wafrica tutaamka na kuanza kutatua matatizo yetu.
ReplyDeleteKipande kutoka Mafinga msitu wa Sao Hill mpk Mbeya barabara ni nyembamba sn mashimo kila mahali. Naulizankwa nini ile barabara mpya iliishia Mafinga mjini ni mipango ya pesa au ndio kila mtu alichukua chake na biashara kuishia hapi
ReplyDeleteHAYA MALORI YANAYO BEBA MAKONTENA SIO YENYE VIWANGO PIA MADEREVA HAWAZINGATII USALAMA WA RAIA MIMI NINGELIWAPA WAZO MALORI YA MIZIGO YAWEKEWE SIKU TATU KWA WIKI KUSAFIRISHA MIZIGO NA MABASI YA ABIRIA SIKU NNE ILI KUEPUSHA WASIKUTANE NAELEWA SIO WAZO RAHISI LAKINI IKIWA HAMJAPATA UVUMBUZI WA HIZI AJALI NI LAZIMA TURUDI NYUMA KATIKA KUFIKIRI. AJALI NYINGI NI BAINA YA MALORI YA MIZIGO NA MABASI HAWA SIO MARAFIKI HIVI VIFO NA SALAAMU ZA POLE TUTACHOKA TUMEZIDI UZEMBE BARABARA KAMA WEMBE BADO ZINAJENGWA MPYA SASA TUJIPANGE KWA KUTOA SALAAM ZA MSIBA SIKU ZIJAZO.
ReplyDeleteMDAU.
KILIONI