Katika adhima ya kufikisha mawasiliano vijijini, Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) imezindua mnara wa mawasiliano ya simu katika kata ya Pagwi, wilaya ya Kilindi Mkoa wa Tanga.

Akihutubia mamia ya wananchi waliohudhuria tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Selemani Liwowa alisema kwa kupata mawasiliano itasaidia wananchi kuwasiliana pamoja na kutafuta fursa mbalimbali kwa ajili maendeleo. Aidha, Mkuu wa Wilaya alisisitiza wananchi kutumia mawasiliano ya simu kwa ajili ya shughuli za maendeleo na usalama wa mali zenu pamoja na nchi kwa ujumla.

“Nawaombeni pia tumieni fursa hii ya uwepo wa mawasiliano kwa ajili ya kukuza uchumi wa Kata hii, kutafuta masoko nje na ndani ya mkoa wa Tanga” alisema Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Selemani Liwowa.

Naye Meneja wa TTCL mkoa wa Tanga alisema kuwa mnara huo unatoa huduma ya mawasiliano katika vijiji vya Lumotio, Pagwi, Makelele, Masilei, Kwekivu na maeneo yote yanayozunguka vijiji hivyo.

Lusama alifafanua kuwa kupitia mfuko unaosimamia utoaji wa huduma ya Mawasiliano kwa wote nchini (UCSAF), TTCL ilipewa jukumu la kufikisha huduma za mawasiliano katika kata 20 kwa awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi wa mawasiliano vijijini. Katika Kata hizo za mwanzo Pagwi ni moja ya Kata zilizonufaika na mradi huo.
Meneja wa Mkoa wa Tanga wa TTCL, Peter Lusama akitoa hotuba siku ya Uzinduzi wa Mnara wa Mawasiliano katika kata ya Pagwi, Wilaya ya Kilindi, Tanga.
Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Selemani Liwowa akizungumza na wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa Mnara wa Mawasiliano wa Pagwi, Wilaya ya Kilindi, Mkoani Tanga. Mnara huu umesaidia wananchi wa maeneo hayo kupata mawasiliano ya simu.
Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Selemani Liwowa akikata utepe, kuashiria uzinduzi rasmi wa mnara wa mawasiliano wa Pagwi, Wilaya ya Kilindi, Tanga.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...