Tume ya Taifa ya Uchaguzi Nchini Tanzania itaanza kusambaza mashine za BVR 248 katika mikoa saba nchni Tanzania Kuanzia katikati mwa wiki ijayo.
Mikoa iliyopangwa kuanza kupokea mashine hizi ni mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa, Wakati zozi likianza mikoa hiyo nyingine zitakuwa zinapelekwa katika mikoa ya Katavi, Mbeya na Dodoma. Mikoa mimgine ni Singida Tabora Geita na Kigoma.

Mkuu wa kitengo cha Ufundi wa idara ya Daftrari/ICT wa NEC Dr Sisit Cariah, Akizungumza na mwandishi wetu amesema kwamba mpaka sasa wanachi wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvumna na Iringa wakae tayari kwani muda wowote watatangaziwa vituo vya kujiandikisha.
 Pamoja na mshine hizo 248 Tume ya taifa ya uchaguzi imewaandaa wataalamu 248 ambao watakuwa na jukumu la kutoa elimu kwa wataalamu wengine 50 kwa kila mmoja nchi nzima kwa ajili ya kuharakisha uandikishaji kwa mfumo wa BVR.
Dr Sisit Ameeleza kwamba wamefanikiwa kufanya maboresho makubwa katika mashine hizi ikiwa ni pamoja na kubadilisha upangaji wa vifaa (settings), mfumo endeshi (Software) na upande wa Vichapishio (printer) ambazo sasa zimetengenezewa Nchini Ufaransa umeboreshwa na nirahisi kusafishwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...