Mkuu wa kitengo cha sheria wa Wakala wa usalama na afya mahali pa kazi(OSHA),Joyce  Mwalubungu, akizungumza na wakandalasi waliohudhuria kwenye warsha iliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mshauri mkuu wa ufundi wa ujasiliamali na miradi kwa vijana Jelous Chirove akizungumza na wakandarasi waliohudhuria kwenye warsha iliyoandaliwa na wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkaguzi mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) akizungumza na baadhi ya wandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano katika jengo la Kazi House jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wakandarasi waliohudhuria kwenye warsha iliyoandaliwa na wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.(Picha zote na Avila Kakingo,Globu ya Jamii)



Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

 MAKANDARASI wametakiwa  kuwajibika kwa kuwahudumia wafanyakazi wao wakiwa sehemu ya kazi kwa kulinda afya na usalama  wakiwa kazini.
Hayo yamesemwa  na Mkaguzi Mkuu wa Wakala wa Usalama na afya  Mahala Pakazi (OSHA),Akwilina Kayumba wakati wa Warsha ya Wakandarasi iliyoandaliwa  na Wakala wa Usalama na Afya sehemu ya kazi  uliofanyika leo katika Ukumbi wa Shirika la Kazi Duniani, jijini Dar es salaam.

Warsha kwa hiyo imelenga kuwajengea uwezo wa Makandarasi  katika kuelekea kuadhimisha siku ya usalama na Afya Mahala Pakazi  Duniani ya afya  Duniani itakayofanyika Aprili 28 mkoani Dodoma.
Amesema sekta ya ujenzi ina wafanyakazi wengi hivyo inatakiwa kuangaliwa kwa ukaribu katika kuepuka ajali ambazo zinaweza kutokea wakiwa kazini pamoja na magonjwa.

Kayumba amesema katika maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahala Pakazi Duniani,Wakala usalama na afya Mahala Pakazi kwa maadhimisho hayo itakuwa  siku ya maombolezo,majeruhi,magonjwa na vifo vya wafanyakazi mahala  pakazi.

Amesema kauali mbiu ya maadhimisho ya siku usalama na Afya Mahala Pakazi  Duniani mwaka huu ikiwa na kauli mbiu ‘Tushirikiane sote kudumisha usalama na afya sehemu ya kazi’.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...