Meneja Uragibishi na Mawasiliano wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Ndugu Philomena Marijani (aliyesimama)akitoa maelezo mafupi kuhusu semina ya siku 5 kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke itayozungumzia uzuiaji wa mimba za utotoni kwa wanafunzi wa wilaya hiyo. Semina hiyo inafanyika katika Shule ya Sekondari Kibasila kuanzia tarehe 13 hadi 17.4.2015.
  Baadhi ya wanafunzi na walimu kutoka Shule 11 za Sekondari katika Wilaya ya Temeke wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Ndugu Donald Chavila (hayuko pichani) wakati alipokuwa akifungua rasmi semina ya siku tano inayozungumzia uzuiaji wa mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Wilaya hiyo tarehe 13.4.2015 kwenye ukumbi wa sherehe wa Kibasila Sekondari.
  Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Bwana Donald Chavila akifungua rasmi semina ya siku 5 ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke. Semina hiyo inaendeshwa na Taasisi ya WAMA, ikishirikiana na Shirika la Engender Health la Marekani na kufadhiliwa na Shirika la Misaada la Serikali ya Marekani,USAID.
Mwanafunzi mshiriki wa semina ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa shule za sekondari katika Wilaya ya Temeke akiwasilisha majibu ya majadiliano ya kikundi chao katika siku ya kwanza ya semina hiyo. PICHA NA JOHN  LUKUWI.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...