Kaimu katibu Tawala mkoa wa Mwanza Bw.Ndaro Kulinjirwa akiongea na Maafisa Vijana,Waratibu wa Ukimwi na Vijana (Hawapo Pichani) kutoka katika Mikoa  ya Simiyu,Shinyanga na Mwanza alipokuwa akizindua rasmi warsha kuhusu Stadi za Maisha kwa washiriki hao leo jijini Mwanza ikishirikisha wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo na Tume ya kudhibiti Ukimwi Tanzania .Warsha iyo ya siku nne  inafanyika katika hoteli ya Midland. Kushoto kwake  ni Mratibu wa Vijana kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bi,Grace Kessy na wa kwanza kulia ni Mtaalamu wa Stadi za Maisha  Bw.Robert Semkiwa.
 Washiriki mbalimbali wa warsha kuhusu Stadi za Maisha wakimskiliza kwa makini Kaimu katibu Tawala mkoa wa Mwanza Bw.Ndaro Kulinjirwa(hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza nao leo jijini Mwanza.Bw Kulinjirwa aliwasisitiza washiriki hao kutumia vyema mafunzo watakayopata ili kubadili maisha yao na ya jamii nzima kwani Stadi za Maisha ndio kinga dhidi ya maambukizi ya Ukimwi.
 Mtaalamu wa Stadi za Maisha Bw.Robert Semkiwa(Aliyesimama) akifurahia jambo na washiriki wa warsha ya siku nne kuhusu Stadi za Maisha  kutoka katika mikoa ya Mwanza,Simiyu na Shinyanga leo hii jijini Mwanza.Warsha hiyo imeanza leo ikiwashirikisha Waratibu wa Ukimwi,Maafisa Vijana na Wadau Mbalimbali.Warsha hii inafanyika katika hoteli ya Midland jijini Mwanza.

Waratibu wa Ukimwi,Maafisa Vijana na Vijana wakiwa katika Picha ya pamoja na Kaimu Katibu tawala Mkoa wa Mwanza Bw.Ndaro Kulinjirwa(aliyekaa mwenye suti ya khaki),Mtaalamu wa Stadi za maisha Bw.Robert Semkiwa(wa Kwanza kushoto aliyekaa),Bi Grace Kessy kutoka Tume ya kudhibiti ukimwi Tanzania  (wa pili kutoka kulia waliokaa) na Bw, Godfrey Masawe ambaye ni Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo(wa kwanza kutoka kulia waliokaa).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...