Vikosi mbali mbali ya Majeshi vikiwa vimejipanga tayari kwa kungia uwanjani kwa ajili ya ufunguzi wa michezo ya majeshi 2015.
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Songea Prof. Nomarn Sigalla King akisalimiana na wachezaji wa timu ya jeshi kutoka Mtwara.

Na Amon Mtega ,SONGEA

MICHEZO ya majeshi inayoshirikisha vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama briged ya kanda ya kusini imefunguliwa rasmi na kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Songea ,Pr Noman sigaa King huku benki ya NMB tawi la Songea likiwa limetoa msaada wa jezi za mpira wa miguu seti saba ambazo zenye thamani ya shilingi 3,000,000.

Akiongea kwenye ufunguzi  huo  uliyofanyika leo katika uwanja wa michezo wa majimaji uliyopo Songea ,Sigara alisema kuwa  michezo hiyo itaimarisha mahusiano ya kiulinzi baina ya mipaka yetu ya Tanzania kwa kuwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama vitakuwa na ushirikiano.

Alisema kuwa ulinzi wa Tanzania katika mipaka yetu  hautegemei jeshi moja tuu bali ni ushirikiano wa vikosi vya majeshi mbalimbali kama vikosi hivi ambavyo vimeshirikishwa kwenye michezo hii iliyozinduliwa na ambayo itarajiwa kufanyika kwa wiki mbili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...