Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Baraka Konisaga akisoma taarifa ya ufunguzi wa mkutano wa kwanza kati ya minane inayotarajiwa kufanyika kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mwanza.
SERIKALI imesema kutokana na Jiji la Mwanza kujengwa nyumba za kudumu bila mpangilio maalumu, imeanza mchakato wa kuainisha maeneo yote ya Wilaya ya Ilemela na Nyamagana yanayounda jiji hilo ili  sehemu makazi, biashara, viwanda na huduma za jamii zifahamike.

Imesema kabla ya kuanisha maeneo hayo, leo itaanza kukutana na  wadau wote na wananchi wa jiji hilo ili kupokea maoni na mapendekezo kabla ya kuanza utekelezwaji wa mpango huo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyolewa jana kwenye vyombo vya habari na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Faisal Issa,imesema  mpango huo umelenga kuondoa migogoro ya ardhi na uvamizi wa maeneo yasiyoruhisiwa.
Wadau wa mkutano kutoka idara za serikali, viongozi wa siasa, waandishi wa habari na wafanyakazi taasisi za umma.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 13, 2015

    Hii hatua ni nzuri, kujenga miji kiholela kuna matatizo yake kwa wakazi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...