Wanafunzi wa kidato cha tatu wa Shule ya Sekondari ya Makumbusho,Mariam Rajabu na Faraja Abdallah wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Vodacom Foundation, Renatus Rwehikiza (kulia) akiwafafanulia jambo kuhusiana na matumizi ya kompyuta mpakato zilizokabidhiwa na mfuko huo kwa kushirikiana na Samsung ikiwa ni msaada kwa wanafunzi wa shule hiyo kuweza kupata mafunzo ya masomo mbalimbali kupitia kompyuta .
Baadhi ya wanafunzi wa wa kidato cha tatu wa Shule ya Sekondari ya Makumbusho jijini Dar es Salaam,Juma Hassan, Fadhil Komba na Francis Mwaimbamba wakijifunza masomo mbalimbali kupitia kompyuta mpakato zilizokabidhiwa na mfuko huo kwa kushirikiana na Samsung ikiwa ni msaada kwa wanafunzi wa shule hiyo kuweza kupata mafunzo ya masomo mbalimbali kupitia kompyuta.
Mkuu wa Biashara Endelevu wa Kampuni ya Vodacom Suraya Hamdulay(kushoto) akifafanuliwa jambo na mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Makumbusho jijini Dar es Salaam, Bernard Yohana, kuhusiana na somo la kompyuta wakati wa kukabidhiwa rasmi kompyuta hizo pamoja na vifaa vya maabara ya kompyuta ikiwa ni msaada uliotolewa na Vodacom Foundation kwa kushirikiana na Samsung kwa ajili ya kupata mafunzo ya masomo mbalimbali kupitia kompyuta shuleni hapo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...