Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Adamu Ng’imba akiwaonyesha waandishi wa habari jinsi mji wa Kisarawe utakavyojengwa, katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo,kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe na Katibu mkuu wa kamati kuu ya Miradi,Mwanamvua Mrindoko na kushoto  ni Afisa Mradi wa Maliasili wa Wilaya ya Kisarawe,Cheyo Nyegele.

Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe
wakimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Adamu Ng’imba alipokuwa akifafanua namna ya mji wa Kisarawe utakavyojengwa,kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo,ambapo wilaya ya Kisarawe inatarajia kuuza viwanja zaidi ya 291 kwa wewekezaji wa viwand.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa  kazini
 Baadhi ya wanahabari kutoka vyombo mbalimbali sambamba na Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Adamu Ng’imba alipokuwa akifafanua namna ya mji wa Kisarawe utakavyojengwa,kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakisoma vipeperushi vinavyoeleza namna ya mji wa kisarawe utakavyojengwa.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kisarawe imetangaza viwanja 291 vilivyopimwa  kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda katika Wilaya hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo  jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Adamu Ng’imba amesema Halmashauri ya Kisarawe ina mazingira rafiki kwa uwekezaji wa viwanda kutokana na maeneo hayo yalivyopimwa.

Ng’imba amesema kuwa mradi wa viwanja hivyo umeshirikisha wananchi wa maeneo hayo ili kuweza kuondokana na migogoro baina ya wawekezaji na wananchi ili kuepuka malengo yaliyokusudiwa yasifanikiwe.

Amesema katika viwanja vilivyopo katika mradi wa viwanda asilimia 63 ya fedha zitazopatikana katika uuzaji wa kiwanja zitakwenda kwa mwananchi ni katika kuepuka migogoro hiyo. Amesema wawekezaji baada ya kukamilisha taratibu zote za umiliki wa ardhi ni miaka mitatu kama ameshindwa kuendeleza Halmashauri itachukua na kuuza kwa mtu mwingine.

Ng’imba amesema katika kuondokana na migogoro na ujenzi holela,Halmashauri imeamua kushirikisha wananchi katika maeneo husika. Amesema watakaopata maeneo ya uwekezaji katika Halmshauri ya Kisarawe watapata hati ndani ya siku saba na wananchi ndiyo watakaonufaika na mradi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...