Na Abou Shatry Washington DC 

 Watanzania walioko nchini Marekani, wamechangisha zaidi ya Dola 3,550 kwa ajili ya kumsaidia ndugu Moh'd Said Moh'd anayehitaji kwenda nchini India kwa matibabu.
Bi Moza Moh'd Khamis akitoa maelezo machache, Maryam Shaaban kulia, pamoja na Bi Asha Haris, Picha zote na (swahilivilla.blogspot.com)

Akifungua shughuli hiyo iliyofanyika May 17, katika Jimbo la Meryland nchini Marekani na kuzijumuisha jumuiya mbali mbali za Kitanzania, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazanzibari nchini humo (ZADIA) Bwana Omar Haji Ali, alisema kwamba mkusanyiko huo ni kielelezo cha umoja, upendo na mshikamano miongoni mwa Watanzania. 

 Katika maelzo yake ya ufunguzi yaliyokamilishwa na dua, Bwana Omar alisisitiza kuwa harambee hiyo iliyofanykika nchini Marekani kwa ajili ya kumsaidia kijana aliyeko Zanzibar, ni uthibitisho kuwa jumuiya za Kitanzania nchini humo zina azma ya kuchangia kidhati katika ustawi wa Tanzania na watu wake.
Mwenyekiti wa Zanzibar Diaspora Association (ZADIA) ndugu Omar Haji Ally akifungua harambee kwa dua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 18, 2015

    Hongereni na endeleeni na moyo wa kusaidia ambao wanahitaji msaada kama huyo kijana.

    Hiyo ni sadaka njema na Inshallah Mwenyezi Mungu atawaongezea kwenye fungu la wema.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...