Mwanakijiji Josephat Lukaza.
Tunapenda Kuchukua nafasi hii kukupongeza kwa kufikisha Miaka kadhaa ya kuzaliwa kwako na ukiwa sehemu ya wanakijiji wa digitali hapa duniani.
Tunachukua nafasi hii kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda na kukubariki kwa kukuongezea maisha marefu na yenye heri hapa duniani ili vizazi vingine viweze kufaidi baraka na neema za mwenyezi Mungu kupitia Wewe.
Leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Kwako iwe chachu na siku ya kufikiria ulipotoka, Ulipo na uendapo ili kuweza kutimiza Malengo yako huku Jamii inayokuzunguka Ikitegemea Mazuri mengi kutoka Kwako.
Ni ngumu kuyatimiza pekee yako lakini tunakuombea kwa Mungu akujalie wepesi katika kutimiza yaliyo mema mbele zake na Jamii inayokuzunguka Umekuwa Mtu ambae ni wa kipekee sana na mwenye kupenda kushirikiana na watu wote pale ambapo unaombwa msaada bila kujali huyu ni nani Mungu Akujalie uendelee na moyo huo huo na mazuri hayo hayo .
Tunakuombea Kwa Mwenyezi Mungu azidi kukupa maisha marefu na yenye Baraka na fanaka tele hapa duniani.
Ukiwa kama Mwanakijiji Mwenzetu tunapenda kukutakia Heri ya Kumbukumbu ya Siku yako ya Kuzaliwa kwa kihispania wanasema 
"Feliz cumpleaƱos Josephat Lukaza"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...