Katibu Mkuu wa CCM ndugu Kinana (kulia) akikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Kata ya Nyehunge Kijiji cha Isaka, Jimbo la Buchosa, wilayani Sengerema, Mwanza leo.
Katibu Mkuu wa CCM ndugu Kinana akitoka akikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Kata ya Nyehunge Kijiji cha Isaka, Jimbo la Buchosa, wilayaniSengerema, Mwanza leo.
Kinana akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyehunge, Jimbo la Buchosa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyehunge, Buchosa baada ya kuzindua mradi wa maji.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara iliofanyika kwenye kijiji cha Nyehunge jimbo la Buchosa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza mmoja wa wakazi wa kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema katika jimbo la Buchosa,alipokuwa akiuliza swali .
Ndugu Kinana ambaye yupo katika ziara hiyo ameambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ameanza ziara mkoani Mwanza, baada ya kumaliza ziara katika mikoa ya Kagera na jana Mkoa wa Geita.
Akiwa mkoani Mwanza atafanya kazi ya kuimarisha uhai wa chama, kusimamia, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusilikiza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema katika jimbo la Buchosa,Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...