Na Bashir Yakub
Makala  zilizopita  nilieleza   mazingira ya  kisheria  ambapo  mtu  anaweza   kunyanganywa  ardhi  yake  na  kufutiwa  hati  miliki  na  hatimye  ardhi  kupewa  mtu  mwingine  au  kukabidhiwa  mikononi  mwa  serikali. Nilieleza  mambo  mengi  ikiwemo   sababu  ambazo  zinaweza  kupelekea mamlaka  za  ardhi  kufuta  hati  miliki  ya mtu.  
Pia  nilionya  kuwa unapomiliki  ardhi  sio  kwamba  umemaliza,  hapana,  isipokuwa  kuna umuhimu  mkubwa wa  kuzingatia  na  kufuata masharti  yaliyo  katika  hati  miliki. Hii  ni  kwasababu  Sheria ya  Ardhi  imeweka  bayana  na  kutoa  mamlaka  kwa  ofisi  kuu  za ardhi  kufuta  umiliki  wa mtu  iwapo  unakiuka  masharti  ya  hati.

Pia  nikaeleza  kuwa  yawezekana  maafisa  ardhi  kutumia  mwanya huo   kuchukua  ardhi  yako  kwa  manufaa fulani  au  kwakuwa  yupo  mtu nyuma  ya  mchezo  huo  ambaye   anaitaka  ardhi  yako. 
Utatumika  mwanya  wa  kutotekeleza  masharti  kukunyanganya  ardhi ili  apewe  huyo  aliyesimamia  mchezo  huo. Na  mwisho  nikasema  kuwa  huwezi  kujua  kama  haya  yapo  mpaka  yakutokee  vinginevyo  unaweza  kudhani   tunaongea  vitu  ambavyo  havijawahi  kutokea. Waliofikwa  na  haya  wanajua  nazungumza  nini. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...