Na  Bashir  Yakub.

Suala  la  mirathi  popote  linapotokea   hutokea  iwapo  kuna  mtu  amekufa  na   ameacha  mali  . Mtu  akishakufa  akaacha  mali  hata  kama  hakuna  ndugu wa kurithi  suala  la  mirathi  lazima  liibuke.  Huibuka kwakuwa  lazima  zile  mali  ziende  pahali  iwe  kwa  mtu  au  kwa  mamlaka. Hata  hivyo  suala  la  mirathi  huibua  hisia  zaidi  hasa  panapokwa  hamna  wosia.  Marehemu  asipoacha wosia  lakini  akaacha   mali  mambo  huwa  sio  mepesi  sana labda  iwe vinginevyo.

  Ifahamike  kuwa mirathi  huhusisha   mambo  mengi. Lakini  pia huhusisha  sheria  nyingi.  Sheria  za kiislam huhusika, sheria  za  kimila  huhusika   na  pia  sheria  za  nchi  ambayo  ni  sura  ya  352. 

1.USIMAMIZI  WA  MIRATHI  KAMA  KUNA  WOSIA.

Kama  marehemu  ameacha  wosia    basi  ni  vema  kuangalia  wosia  huo  umemtaja  nani awe  msimazi wa  mirathi. Hili  ni muhimu  watu  walijue  hata  wale  walioandika  wosia  tayari au  wanaotarajia  kuandika  wosia.  Wengi  wamekuwa  wakiandika  wosia  na  kugawa  mali  lakini  wakisahau  kuteua  na  kumtaja  msimamizi  wa  mirathi  wakiamini  kuwa  kila  mtu  atakapochukua  chake   mambo  yataishia  hapo. 

Laa  hasha  mambo  si  mepesi  kiasi  hicho.  Kwa  hiyo  yafaa  kuangalia  nani  ametajwa  kama  msimamizi  wa  mirathi  katika  wosia    na  huyu  ndiye  atakuwa  msimamizi  wa  mirathi. Ikiwa  wosia  upo  lakini  haukumtaja  msimamizi  wa  mirathi  basi  taratibu  za  kimahakama  nitakazoeleza  hapa  chini  zitafuata.

2.  KUMTHIBITISHA  MSIMAMIZI  WA  MIRATHI  MAHAKAMANI.

Ikiwa  wosia   umemtaja  msimamizi  wa mirathi  basi  hilo  tu  halitoshi. Sheria  inataka  msimamizi  wa  mirathi  athibitishwe  pia na  mahakama. Hii  ni  kwasababu   mahakama  hutoa  hati  maalum   kwa  aliyethibitishwa kuwa  msimamizi  wa  mirathi  ambayo  hutum ika  sehemu  zote  za  kisheria  kwa  mfano  kuchukua  hela  za  marehemu  benki, kuchukua  hisa za  marehemu, kuuza  na  kununua  mali  za  marehemu,kubadilisha  vitu  kama  hati na kila  kitu  ambacho  huhusisha  taratibu  maalum  za  kisheria. Kwakweli  isingewezekana  kutumia wosia  kwa kuuonesha  kila ofisi  unayoingia  katika kufanya  michakato  hii yote.  Na  hapa ndio  mahitaji  ya  kuthibitishwa  na  mahakama  na  kupata  hati maalum ambayo  ni  kama  utambulisho  yalipotokea. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...