Na  Bashir  Yakub
Wiki  kadhaa  zilizopita   nilipigiwa  simu  na  mama  mmoja  akitaka  nimpe  ushauri  wa  sheria  kuhusu  jambo  fulani. Nilifanya  miadi  naye   na tukafanya  mazungumzo. Kubwa  kuhusu  shida  yake  ilikuwa  ni  tatizo  la  mkopo ambapo  benki  moja imeuza  nyumba  yake  maeneo  ya  Kinondoni  Dar  es  saaam.  Wasiwasi  wake  ulikuwa  ukiukwaji  wa  taratibu  za  mauzo  ya  nyumba  yake  na  hivyo  akitaka  kujua  afanye  nini. Maswali  yake  yalikuwa  mengi  na  nilimjibu  kwa  kiwango  cha  juu.
Pamoja  na  hayo  kilichokuwa  kikimpa  shida  sana   na  kuamini  kuwa  kulikuwa  na  mchezo  mchafu  umefanyika  katika  uuzwaji  wa  nyumba yake  ilikuwa  ni   hatua ya  benki  inayomdai  kujiuzia  nyumba  yake   katika  mnada  wa  hadhara. Alidai  hakuwahi  kuona  mdai  deni  anajiuzia  mali  iliyowekwa kwake kama   dhamana. 
Alidai  anavyojua   ni  mnada  kutangazwa  na  wenye  nia  hujitokeza  kununua  na  kati  ya  hao  mdai  hawezi  kuwa  mnunuzi.  Aliamini  hatua  ya  mdai  kuwa  ndiye  mnunuzi  ulikuwa  ni  mchezo  uliopangwa  ili   kuchukua  nyumba  yake.  Nilimuuliza  kilichomuudhi  zaidi  nini  kwani  sioni  tofauti  kati  ya  mtoa  mkopo  kujiuzia  mwenyewe na  kununua  mtu  mwingine  kwani  kuuza  ni  kuuza  tu.  

Akanieleza ukweli  kuwa  wao  walishampanga ndugu  yao  ambaye  angeweza  kununua  na  kwakuwa  ni  ndugu  kuna  mipango  yao  kama  familia   walishaipanga.  Kwa  hiyo  alihisi  ilifanyika  hila  ili  wao  wasiichukue  tena  nyumba  hiyo  kwakuwa  mdai  naye  alikuwa  akiitaka kwa  udi  na  uvumba . Nilimpa  ushauri  ambao  ningependa  pia  kuushiriki  na  watu  wengine   kupitia  makala  haya   ili  faida iwe  kubwa. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...