JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
 TANGAZO KUHUSU USHIRIKI WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII  KWENYE MAONYESHO YA 39 YA  BIASHARA YA KIMATAIFA YA DARES SALAAM
  1. Wizara ya Maliasili na Utalii inashiriki kwenye Maonyesho ya 39 ya  Biashara ya Kimataifa ya Dares Salaam (Saba Saba) yatakayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius.K.Nyerere,  Barabara ya Kilwa kuanzia tarehe 28 Juni hadi 8 Julai, 2015.
  2. Karibu kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii ujionee na kuelimika kuhusu shughuli za Utalii,  Ufugaji Nyuki, Uhifadhi wa Misitu, Malikale na Wanyamapori.
  3. Safari za kutembelea Hifadhi za Mikumi na Saadani kwa gharama nafuu zitakuwepo
  4. Aidha, Wizara itachezesha bahati nasibu ambapo mshindi atazawadiwa safari ya kwenda kutembelea Hifadhi ya Mikumi au Saadani.
  5. Pia, Utapata fursa ya kuwaona wanyamapori hai kama vile Chui, Mamba, Nyoka, Ndege wa aina mbalimbali pamoja na mfalme wa pori SIMBA.
Karibuni Wote
“Unganisha Uzalishaji    na Masoko ”




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...