Na Benjamin Sawe,Maelezo

Mabadiliko katika sekta ya hifadhi ya jamii nchini yamepelekea kuwepo na mabadiliko ya sheria ya mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma (PSPF). Sheria ya Mfuko wa pensheni wa PSPF sasa inaruhusu kusajili wanachama katika sekta zote za umma na binafsi. Na kwa sasa mfuko una mipango miwili ya uchangiaji wa lazima yaani PSPF Mandatory Scheme na mpango wa uchangiaji wa hiari yaani PSPF Supplementary Scheme

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwandishi wa Makala hayaBi Mwanjaa Sembe, Meneja Mpangowa Uchangiaji wa Hiari PSPF anasema uwasilishaji michango kwa kutumia huduma ya MaxMalipo itawasaidia wachangiaji kupata huduma za michango yao.

Anasema huduma ya kulipia kupitia mfumo wa Maxmalipo imeanzishwa na mfuko wa pensheni wa PSPF kwa ajili ya kupanua wigo kwa wanachama wa mfuko huo kuchangia na kujua salio la michango yao popote walipo ambapo huduma hiyo itawarahisishia watumiaji kutosafiri kwa umbali mrefu ili kupata huduma hiyo.
Mfuko umeona adha na shida walizokuwa wanazipata wateja wetu ndio maana tukaamua pamoja na huduma nyingine zitolewazo na mfuko wetu tujiunge na wenzetu wa Kampuni ya MaxCom inayotoa huduma ya Max Malipo ili kuweza kuwakomboa wateja waweze kuchangia pamoja na kujua kiasi cha michango yao kwa urahisi kwa kutumia huduma hiyo hivyo kuwafanya kuwa na muda mrefu wa kutafuta kipato badala ya kusafiri kwa umbali mrefu kufuata huduma.Anasema Bi. Sembe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...