RAIS wa Shirikiso la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi ameteua Kamati ya ushauri ya Ligi Kuu (VPL) na ligi Daraja la Kwanza (FDL) nchini.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo ni Alhaj Ahmed Mgoyi na katibu wa Kamati ni mtendaji mkuu wa Bodi ya Ligi nchini (TPLB) na wajumbe wengine saba.

1. Alhaji Ahmed Idd Mgoyi (Mwenyekiti)
2. Boniface Wambura (Katibu)
3. Kennedy Mwaisabula- Mjumbe
4. Idd Mshangama- Mjumbe
5. Amiri Mhando- Mjumbe
6. Grace Hoka- Mjumbe
7. Ibrahim Kaude (Vodacom)- Mjumbe
8. Baruan Muhuza (Azam Media)- Mjumbe
9. Peter Simon- Mjumbe

Kazi za kamati hiyo zitakua ni:
(i) Kufuatilia mwenendo wa Ligi
(ii) Kuishauri Bodi/TFF namna ya kuboresha Ligi
(iii) Masoko
(iv)  Leseni za Vilabu (Club Licensing)
(v)  Mipango ya Maendeleo ya Vilabu
(vi) Viwanja vya mazoezi
(vii) Utoaji wa tuzo za ligi mbalimbali
(viii) Kutengeneza vigezo (criteria) vya washindi wa tuzo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Kwa mala ya kwanza TFF imefanya uteuzi usiokuwa na picha ya utabaka.

    ReplyDelete
  2. Kwa mala ya kwanza TFF imefanya uteuzi usiokuwa na picha ya utabaka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...