Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama, wakati wa kuufunga Mkutano huo jioni hii kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM (Dodoma Conveition Centre), uliopo Mjini Dodoma. CCM wanafanya mkutano mkubwa wa kumtambulisha Mgombea wao jioni hii kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwatambulisha Mgombea Urais wa CCM, Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mgombea Mwenza, Mh. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuufunga Mkutano huo.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin Mkapa akimkumbatia Dkt. John Pombe Magufuli wakati akimpongeza kwa ushindi alioupata.
Mgombea Urais wa CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Mzee Pius Msekwa na Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...