Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii

VIONGOZI nchini wametakiwa kushiriki katika mkutano wa mabadiliko ya tabia ya nchi utakaofanyika Julai 13 na 16 Addis Ababa Ethiopia.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Mratibu wa Mtandao wa Mabadiliko ya Tabia ya Nchi (CAN),Sixsbaty Mwanga amesema mkutano huo ni muhimu kutokana hali iliyopo sasa katika mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kuongezeka ukame ,njaa pamoja na mafuriko, hivyo viongozi wanaweza kushawishi mkutano katika kuongeza bajeti katika eneo hilo katika kukabiliana na majanga hayo.

Amesema fedha ya kuweza kupambana na mabadiliko hazitoshi kufikia mwaka 2020, Tanzania kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi itatumia Trilioni mbili  kwa mwaka kutokana na ambayo itakuwa imefikia katika mabadiliko ya tabia.

Mwanga amesema fedha za mabadiliko ya tabia ya nchi zinatakiwa ziwekwe wazi ili kusaidia wananchi kuweza kupata msaada pale panapotokea majanga ya ukame na mafuriko na waketi mwingine fedha hizo zinapotea na kushindwa kutatua matatizo yanayotokana  na mabadiliko hayo .

Amesema mikutano iliyopita haikuwa na changamoto ya tabia ya nchi lakini sasa tatizo limezidi kukua kutokana na hali iliyopo kufikia mwaka 2020 vifo vitakuwa vya kila siku vinavyotokana na mabadiliko hayo.

Amesema katika malengo 17 ya maendeleo endelevu ya masuala ya tabia ya nchi yanatakiwa kuangaliwa kwa katibu katika kila kpengele katika kuweza kukabili hali hiyo.

Hata hivyo CAN inatarajia kufanya maandamano  ya matembezi  amani Julai 12 ambayo itashirikisha zaidi ya wadau 400 wa mazingira kushiriki na kupaza sauti, na matembezi hayo yataanzia katika chuo Kikuu cha Ardhi (ARU) na kuishia katika kiwanja cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mratibu wa Mtandao wa Mabadiliko ya Tabia ya NCH I(CAN) ,Sixsbaty Mwanga akizungumza na waandishi  wa habari (hawapo pichani)  katika mkutano wa mabdiliko tabia nchi katika kuelekea mkutano wa viongozi utaofanyika nchini Addis Ababa,Ethiopia uliofanyika leo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 
Baadhi ya waandishi wakifatilia taarifa Mratibu wa Mtandao wa Mabadiliko ya Tabia ya NCHI(CAN) ,Sixsbaty Mwanga hayupo pichani katika mkutano uliofanyika leo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...