Na
Bashir Yakub.
Wakati nilipoandika kuhusu
talaka
na mambo yanayokubalika kisheria
kama sababu za
talaka nilipata maoni
na maswali mengi kutoka kwa wasomaji wetu. Kati
ya hao ni mmoja
ambaye alijitambulisha kwa
jina na kuwa
ni mkazi wa kinondoni Dar es
salaam. Huyu aliuliza swali
lake ambalo ndilo
kichwa cha makala
haya. Alisema ameziona
sababu nilizoeleza ambazo
zinapelekea mtu kupewa
talaka lakini sababu
inayohusu tatizo lake
hakuiona na hivyo
aliomba nimpatie ufafanuzi. Maelezo yake
kwa ufupi yalikuwa
hivi:
1.KUPATA MIMBA
NJE YA NDOA.
Ndugu huyu alichoeleza
ni kuwa yeye ni
muajiriwa katika jeshi la
Wananchi wa Tanzania.
Na kuwa mwaka
jana alipangiwa safari
ya kikazi kwenda Congo
kwa ajili misheni
maalum ya jeshi
kwa kipindi cha
miezi sita. Anasema
alikwenda na kumuacha mke
wake nyumbani kwake
ambapo amerudi mwaka
huu .
Anasema ndani
ya wiki moja
tangu arudi hakuielewa
hali ya mke
wake kitu kilichomfanya achukue
maamuzi ya kumpeleka
hospitalini kwa ajili
ya vipimo. Alifanyiwa
vipimo vyote na
hatimaye kugundulika ana
mimba ya mwezi mmoja. Swali
la ndugu huyu
lilikuwa ni sheria inasemaje
katika hali kama
hiyo. Kusoma zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...