Mwandishi wa makala haya Bw. Yusuph Kileo akitoa mada kwenye moja ya vikao vya usalama mitandao jijini Nairobi, Kenya, hivi karibuni
Nimekamilisha vikao vya usalama mitandao vilivyofanyikia jijini Nairobi kufuatia mualiko maalum nilioupata. Katika vikao hivyo niliwasilisha mada mbili (ya kwanza ikiwa ni namna ya kukabiliana na uhalifu mtandao na mada ya pili ikiwa ni namna ya uchunguzi wa makosa ya digitali kitaalam) katika mada hizo mbili ambazo zilipokelewa vizuri na kupelekea mijadala ya kipekee kuna mengi  nikajifunza kutoka kwa washiriki.

 Aidha, nilishiriki mijadala duara iliyojikita katika changamototo mbali mbali za uhalifu mitandao na kuiangazia sharia mtandao ya nchi ya Kenya.
Kenya ni miongoni mwa nchi tatu barani afrika ambazo zimeorodheshwa kuwa na uhalifu mkubwa sana wa kimtandao nyingine ni Nigeria pamoja na Afrika ya kusini. 

Tukijadili takwimu za kutisha duniani kote, tulishuka na kuangazia bara la Afrika na baadae Afrika mashariki na hatimae kujikita na takwimu za nchi ya Kenya.

Kwa upande wa Kenya kwa mujibu wa takwimu zilizo wasilishwa katika mkutano, hadi kufikia Mwezi wa saba mwaka huu (2015) kuna simu 34.8 Milioni  huku watumiaji wakiwa ni 26.0 Milioni. Aidha, matumizi ya intaneti ni 29.1 milioni ambayo ni sawa na 65% “penetration”. Takwimu hizo zinasindikizwa na upotevu wa dola za kimarekani 20 milioni ($20 Mil) kila mwaka kutokana na uhalifu mtandao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ndugu Kileo,

    Hongera kwa kutuwakilisha, na shukrani kwa taarifa. Huwa napenda kujifunza mambo mapya, na kwa msingi huo umenipa changamoto. Nakutakia kila la heri.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...