MGOMBEA Ubunge wa jimbo la
Iringa Mjini kupitia ACT Wazalendo Bi Chiku Abwao(pichani) amesema heri ya miaka
mitano ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Mobica Mbega ( CCM) kuliko
miaka mitano ya Mchungaji Peter Msigwa ( Chadema)hivyo ametawa mwaka huu
wananchi kumchagua yeye
Akizungumza
katika mkutano wake wa kampeni za Ubunge jana kata ya Kihesa alisema
iwapo atakuwa mbunge wao atahakikisha anakuwa mbunge wa mfano wa
kuwaletea maendeleo sahihi.
Kwani
alisema kuwa historia ya jimbo hilo mwaka 1995 walichagua NCCR mageuzi
ambapo Bw Mfalamagoha Kibasa kuwa mbunge ila baada ya kushindwa
kutekeleza ahadi zake mwaka 2000 walimchagua Monica Mbega ( CCM) ambae
kipindi cha kwanza alifanya Kazi vizuri na mwaka 2005 wananchi
walimchagua tena ila hakuweza kufanya Kazi ndipo walipomchagua Mchungaji
Peter Msigwa( Chadema) ambae hajafanya Kazi yoyote.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...