Asali ikiwa imechanganywa na mdalasini tayari kwa matumizi
Wadau wetu wale ambao wanasumbuliwa sana na CHUNUSI iwe USONI, KIFUANI, MGONGONI n.k wanaweza tumia mchanganyiko mzuri wa ASALI na MDALASINI WA UNGA kwa kupaka angalau mara moja kwa siku.
ASALI na MDALASINI zinasaidia kuponyesha kwasababu zina tabia za ANTI-BACTERIAL( zinaua na kuzuia mazalia ya bacteria)
Jinsi ya kufanya:-

1. Chukua vijiko vitatu(3) vya chai vya ASALI
2. Chukua nusu kijiko cha chai cha MDALASINI WA UNGA safi
3. Changanya pamoja kupata uji uji mzuri
4. Paka sehemu yenye chunusi na kisha kaa nayo kwa angalau dakika 10-30 kisha osha kwa maji ya uvuguvugu.
ANGALIZO: MDALASINI unaweza kuwasha kwenye ngozi hivyo unashauriwa ujaribu kupaka kidogo kwenye kiganja cha mkono kwanza ili kupata uhakika kua haitakusumbua.
(Imeandaliwa na Honey Spring na Jamiimojablog)
 0683370065 au 0769129351

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...