Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inafanya mkutano wa siku tano kati ya Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Kenya ili kuimarisha na kuhakiki mipaka kati ya nchi hizo. Kikao hicho cha wajumbe maalumu kutoka nchi hizo mbili kinafanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 14 hadi 18 septemba 2015.
Mkurugenzi Idara ya upimaji na Ramani Bw. Justo Lyamuya, Mkurugenzi wa Nyumba Bw. Charles Mafuru kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Balozi wa Kenya nchini Tanzania Mhe. Chirua Ali wakiwa katika kikao hicho.
Wajumbe kutoka Tanzania na Kenya wakiwa katika kikao hicho
Washiriki wa mkutano wakiwa katika picha ya pamoja, hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Picha na Hassan mabuye.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...