HOSPITALI ya Taifa Muhimbili –MNH-  imetoa  mafunzo kwa watumishi wake kudhibiti  ugonjwa wa kipindupindu   ambao  umesambaa na kusababisha watu 989 kuambukizwa  ugonjwa  huo  jijini Dar es salaam.

Mafunzo hayo ya siku saba ambayo yanahusisha Wakurugenzi, Wakuu wa Idara , Madaktari, Wauguzi , Wafamasia pamoja na Wahudumu  yana lengo la kuwaelimisha juu ya ugonjwa huo , jinsi ya kuzuia , kumtibu mgonjwa na kumtambua mtu mwenye dalili za Kipindupindu.

Akielezea  mafunzo hayo Mkuu wa Idara ya magonjwa ya dharura na ajali  ambaye  pia  ni Daktari Bingwa wa magonjwa  hayo  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili  Dokta  JUMA   MFINANGA amesisitiza kuwa chanzo kikuu cha ugonjwa wa Kipindupindu ni uchafu lakini pia maji  machafu yanachangia kwa asilimia kubwa kuenea  kwa ugonjwa huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. SIKU SABA KUFUNDISHWA JINSI YA KUZUIA KIPINDUPINDU, HUU NI UPUUZI MTUPU. KIPINDUPINDU NI UGONJWA WA UCHAFU. MTU AKILA MAVI NDO ANAUPATA, NA MAVI SIYO LAZIMA YAONEKANE, KWANI KWENYE MAJI MACHAFU, VYAKULA VICHAFU, MIKONO MICHAFU, VIPOLO VICHAFU, CHA MAANA NI USAFI BINAFSI NA MAZINGIRA. VIBRIO CHOLERAE ANAPENDA UCHAFU. HUITAJI SIKU SABA KUWAFUNDISHA WATU WAZIMA KUHUSU CHOLERA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...