Nuh Mziwanda amewataka wasanii kuwa
wazalendo kwa kuonyesha hisia zao za vyama vya siasa na kuonyesha
ushirikiano katika kuhamasisha.
Akizungumza na Planet Bongo ya East Africa Radio leo, Nuh alisema maendeleo yatakayopatikana ni manufaa kwa watanzania wote kwa ujumla.
“Wewe ukiwa msanii sio kwamba sio mwananchi wa kawaida,” alisema.
“Wewe pia unahitaji kutawaliwa vizuri. Unahitaji utawala mzuri ambao utaongoza hata kazi zako ziende vizuri.
Akizungumza na Planet Bongo ya East Africa Radio leo, Nuh alisema maendeleo yatakayopatikana ni manufaa kwa watanzania wote kwa ujumla.
“Wewe ukiwa msanii sio kwamba sio mwananchi wa kawaida,” alisema.
“Wewe pia unahitaji kutawaliwa vizuri. Unahitaji utawala mzuri ambao utaongoza hata kazi zako ziende vizuri.
Kwahiyo ni vyema mtu ukajua upo upande gani, huo ni upendo wa
nchi yako na ni mzalendo. Kila binadamu anapenda uongozi mzuri ndio
maana kila mtu akiwa na akili timamu ana haki ya kuchagua chama
anachokitaka,” aliongeza.
“Lakini sisi wasanii tusijisahau tukawa tunashindwa kuweka hisia zetu kwaajili ya maslaHi ya nchi yetu. Unaogopa kuweka wazi wewe ni chama gani, unampenda mwanasiasa gani! Sisi ni vioo vya jamii tunaangaliwa pia na watu na kuna watu wahitaji ushauri au ufafanuzi juu ya viongozi waliotangaza nia. Kwa sisi inatubidi tuwe mfano kwanza kabla ya wananchi.”
“Lakini sisi wasanii tusijisahau tukawa tunashindwa kuweka hisia zetu kwaajili ya maslaHi ya nchi yetu. Unaogopa kuweka wazi wewe ni chama gani, unampenda mwanasiasa gani! Sisi ni vioo vya jamii tunaangaliwa pia na watu na kuna watu wahitaji ushauri au ufafanuzi juu ya viongozi waliotangaza nia. Kwa sisi inatubidi tuwe mfano kwanza kabla ya wananchi.”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...