Wimbo maalum wa kuhimiza amani kabla na baada ya uchaguzi mkuu, utawekwa rasmi hadharani mbele ya waandishi wa habari Jumanne hii.
 Wimbo huo uliopewa jina la “Amani Kwanza” utapigwa ‘live’ kwa mara ya kwanza mbele ya wana habari ndani ya ukumbi wa nyuma wa Mango Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam kuanzia saa 6 mchana. 
“Amani Kwanza” ni ngoma iliyopigwa katika miondoko ya rhumba ikiwa imeshirikisha nyota wengi wa muziki wa dansi chini ya umoja  wa muda wa wanamuziki wa dansi na taarab. 
Mgeni rasmi katika tukio hilo anatarijiwa kuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni bwana Paul Makonda. 
Mratibu wa ‘project’ hiyo Juma Mbizo alisema umoja huo haufungamani na dini, kabila wala chama chochote na kwamba lengo la ni moja tu – kusumbaza ‘mahubiri’ ya amani, umoja na mshikamano kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu. 
Mbizo amefafanua kuwa wimbo huo umerekodiwa katika studio za Sound Crafters chini ya producer Enrico huku video ikiwa imefanywa na King Dodoo. 
Wanamuziki waliotengeneza wimbo huo wako chini ya kamati inayoongozwa na Kanku Kelly ambaye ni mwenyekiti, katibu Omar Teggo, wajumbe ni Mafumu Bilal, King Dodoo na King Kiki huku Juma Mbizo akiwa mjumbe na mratibu. 
Mbizo amesema baada ya utambulisho huo, kila mwanahabari atapatiwa CD na DVD moja ya wimbo huo. 
“Lengo letu ni kutaka wanahabari wawatambue wasanii wote walioshiriki kutengeneza wimbo huo ikiwa ni pamoja na kuusikiliza ‘live’ hivyo naomba waandishi wa habari na wadau wa muziki waje kwa vingi Mango Garden Jumanne mchana,” alisema Juma Mbizo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...