Bendera ya  Palestine itapepea nje ya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa,   hii inafuatia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  kupitisha azimio ambalo linatoa fursa kwa nchi ambazo si  mwanachama kamili wa Umoja huo  kupeperusha bendera yake Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Ubao wa Matangazo ndani ya Ukumbi Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  ukionyesha matokeo ya kura katika tukio la kihistoria  kufanyika ambapo Baraza hilo  limepitisha azimio linalotoa fursa kwa Palestina kupeperusha bendera yake. Nchi wanachama walipiga makofi kushangilia kupitishwa kwa azimio hilo, ambalo Israel imesema Palestina inatafuta umaarufu kwa njia za mkato badala  ya kurejea kwenye meza ya mazugumzo.
 
Na Mwandishi Maalum New York
BARAZA Kuu la Umoja wa Mataifa,  jana Alhamis, limepitisha Azimio ambalo kwa mara ya kwanza   tangu kuanzishwa kwa Umoja huo, litaruhusu nchi ambazo  siyo  mwanachama kamili kupeperusha  bendera yake katika  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.

Kupitishwa kwa azimio hilo ambalo  limepigiwa kura  za ndiyo 119 za hapana  nane  na zisizofungamana na upande wowote 45 kunaipa   fursa Palestina kupeperusha  bendera yake nje ya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.

Mara baada ya  matokeo ya kura kutangazwa rasmi, Wajumbe wa Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa walipiga makofi kama ishara ya kufurahia kupitishwa kura nyingi azimio hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...