New Picture
Familia ya marehemu Dr. John Edward Mchechu wa Ukonga Dar es salaam wanapenda kutoa shukrani zao za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki walioshirikiana nao na kuwafariji kwa hali na mali katika kumuuguza na mpaka kumlaza katika nyumba ya milele mpendwa baba yao Dr. John Edward Mchechu aliyefariki tarehe 21/07/2015 nyumbani kwake Ukonga na kuzikwa tarehe 26/07/2015 Muheza, Tanga.
Shukrani za pekee zimfikie Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. JakayaMrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal, WaziriMkuu, Mh. Mizengo Peter Pinda, Mawaziri, Wabunge, Wakuu wa Mashirika na Wafanyakazi wa Serikali kwa kutufariji kipindi chote cha kuumwa kwake mpaka alipotwaliwa kutoka ulimwengu huu.
Shukrani za pekee pia ziwafikie wafanyakazi na wajumbe wa bodi ya NHC, Serengeti Breweries, DAWASCO, KCB, Rafiki Club, Soul Sisters, New Millenium Women Group, Beach Ladies, Sisters Club, Madaktari na wauguzi wa hospitali za Muhimbili, Hindu Mandal, Apollo Hydrabadna Dispensary yaArafa.
Mapadri na wachungaji wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Mbezi Beach, Makanisa ya Anglikana ya Mtakatifu Paulo la Ukonga, Dar es Salaam na Mtakatifu Petro la Mkuzi,Tanga, kwaya mbalimbali na vikundi vya maombi kwa msaada wao wa kiroho.
Tunawakushukuru mtu mmoja mmoja lakini haiwezekani kwani watu ni wengi sana, tunaomba tu mpokee shukrani zetu za dhati kutoka moyoni mwetu kwajinsi mlivyotufariji katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa baba yetu.
Misa ya Shukrani
Familia ya marehemu Dr. John Edward Mchechu wanapenda kuwakaribisha wote katika misa ya shukrani itakayofanyika siku ya Jumamosi tarehe 12/09/2015 kuanzia saa mbili asubuhi katika kanisa la Mtakatifu Petro Mkuzi, Tanga. Karibuni sana mjumuike nasi.
Raha ya milele umpeeeh Bwana wamilele umwangazie apumzike kwa amani, Amina
MR. & MRS. NEHEMIAH MCHECHU.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...