MUIMBAJI nguli wa muziki Afrika, Solly Mahlangu anatarajia kuwasha moto kwenye jukwaa la Tamasha la Amani ambalo litarajia kufanyika Oktoba 4 uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama mwimbaji huyo ndiye atakayekoleza maombi ya amani ya Tanzania ambayo inapigiwa chapuo la kulindwa kila kukicha.
 
Msama alisema hivi sasa Kamati yake inaendelea na maandalizi ya kufanikisha tamasha hilo ambalo ni chachu ya amani hasa kuelekea uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25 kwa nafasi za urais, Ubunge na Udiwani.
 
Aidha Msama alisema Kamati yake inaendelea na mawasiliano na waimbaji wa nchi za Rwanda, Uganda, Kenya, Burundi na Uingereza ambazo ni mojawapo ya nchi ambazo ni kichocheo cha  amani ya Tanzania.
 
“Kwa kuwa tumejipanga kumpigia magoti Mungu ili kuilinda amani yetu, hatuna budi kuwashirikisha pia wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali  sambamba na waimbaji ambao watakaoimba nyimbo ambazo zitachochea amani,” alisema Msama. 
 
Msama alisema tamasha hilo litahudhuriwa na viongozi wa kada ya siasa ambao watakuwa ndio walengwa ambao wanatakiwa kutoa somo kwa vijana ambao wamejikita katika siasa bila ya kuwa na weledi wa siasa.“Tutakuwa na matukio mengi ambayo ni viashiria vya kuombea amani Tanzania ambako pia kutakuwa na tuzo maalum ambazo watakabidhiwa baadhi ya viongozi ambao mchango wao katika jamii,” alisema Msama.

Mwisho      

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...