Haya ndiyo  Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu (Ajenda 2030) ambayo  leo Ijumaa Wakuu wa Nchi na Serikali wanayapitisha katika Mkutano wao wa Kihistoria  Unaofanyika  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani. Ajenda 2030 ambayo utekelezaji wake unaaza mwakani inachukua nafasi ya  Malengo ya Maendeleo ya Millenia( MDGs) ambayo yamefikia ukiongoni mwaka huu.  Upitishaji wa Ajenda 2030 utatanguliwa na hotuba ya Baba Mtakatifu Francis 
 Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi  Liberata Mulamula akizungumza wakati wa mkutano ulioandaliwa  kwa pamoja  na  Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani na Mashirika  ya Kimataifa kama vile Mpango wa Chakula Duniani, Mkutano uliokuwa ukijadili changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na uhusiano wake na usalama wa chakula,  lishe na afya. Mkutano huu ulifanyika  siku ya alhamis katika Uwakilishi wa Kudumu wa Ujeruman katika Umoja wa Mataifa
 Sehemu ya washiri wa mkutano  kuhusu uhusiano wa mabadiliko ya tabia nchi na athari zake kwa usalama wa chakula,  lishe na afya wakimsikiliza Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula ambaye alikuwa kati ya wanajopo watano waliozugumza katika mkutano huo.

Na  Mwadishi Maalum, 
New York
 Leo   Ijumaa,   Viongozi  Wakuu wa Nchi  na  Serikali zaidi  ya 150  kutoka mataifa mbalimbali duniani,  watapisha ajenda na malengo mapya   ya  maendeleo endelevu  ( Ajenda 2030)  kuchukua  nafasi ya  Malengo ya Maendeleo ya Millenia yanayomaliza  muda wake mwishoni mwa  mwaka huu.
Katika mkutano huu wa kihistoria  unaofanyika  miaka kumi na tano tangu MDGs zilizopitishwa, utatanguliwa  na hotuba ya  Baba Mtakatifu   Francis.
 Baada ya  kupitisha ajenda 2030 na ambayo imejikita zaidi katika kuutokomeza  umaskini na  ulinzi wa mazingira pasipo kumwacha yeyote nyuma,Viongozi   hao Wakuu  wa Nchi na Serikali   kila mmoja wao atapata fursa  ya kuelezea matarajio ya serikali yake katika utekelezaji wa ajenda hiyo yenye malengo 17.
Tayari   Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali  wamekwisha kuwasili Jijini New York , yaliko Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  unaongozwa na  Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
 Siku moja  kabla ya  kupitishwa kwa ajenda 2030, baadhi ya viongozi ambao wameambatana na  Mhe. Rais wameshiriki katika mijadala mbalimbali na ambayo maudhui yake yanashabihiana na   ajenda nzima ya  Maendeleo Endelevu.
Akiwakilisha ujumbe wa  Tanzania katika mikutano hiyo ya pembezoni,  Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi  Liberata Mulamula, alishiriki katika majadiliano kuhusu  mabadiliko ya tabia nchi na  uendelevu wa   usalama wa chakula, lishe na  Afya
Balozi Mulamula alikuwa  kati ya wanajopo watano katika majadiliano hayo  ambayo   yaliandaliwa na  Wizara ya  Ushirikiano wa Kiuchumi na  Maendeleo ya  Ujerumani na Mashirika ya Kimataifa .
Katika  majadiliano hayo ambayo yalijikita katika kuangalia ni namna gani  utekelezaji wa  ajenda ya  maendeleo endelevu  unavyoweza kuathiriwa na  mabadiliko ya tabia nchi na hususani katika maeneo yanayomgusa mwananchi wa kawaida kama vile usalama wa chakula, lishe na afya.
Aidha  wanajopo hao  walitakiwa kujibu  hoja mbalimbali zikiwamo  ni kwa namna gani kwa mfano Tanzania imejiandaa katika kukabiliana na  mabadiliko ya tabia  nchi na ambayo kwayo kwa namna  moja ama nyingine yanaweza kuleta  au yanasababisha  matatizo katika  eneo kama kilimo na lishe.
Akijibu hoja hiyo pamoja na nyingine,  Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula  aliwaeleza  washiriki wa majadiliano  hayo kwamba kwa nchi kama  Tanzania mabadiliko ya tabia nchi ni  jambo lililo dhahiri na si nadharia.
Akatoa mfano kwa kusema kwamba,  kuna  baadhi ya  maeneo ya nchi,  ambapo wakulima wanashindwa kutambua msimu halisi wa kuanza kulima   na kupanda  tofauti na miaka  ya nyuma.
Aidha akasema,  maeneo mengine mvua zinanyesha kupita kiasi na wakati  maeneo mengine yana kumbwa na ukame wa kupindukia na hivyo kuathiri shughuli za kilimo na hatimaye ukosefu wa chakula na  chakula chenye viini lishe  ambavo ni muhimu kwa ukuaji na maendeleo  hususahi ya watoto chini ya  miaka mitano.
Mfano mwingine ambao  anasema ni wazi  umechangia  kwa namna moja ama nyingine katika ubaribufu wa mazingira ni pamoja na matumzi  yasiyo endelevu ya ardhi, ukataji wa   holela   wa miti na ile hali ya  mito  mikubwa kupingukiwa  maji na hivyo kufanya mabwana makubwa  yanatuyotumika kuzalisha umeme kukosa maji ya kutosha.
“Nilipokuwa mdogo tulikuwa tunakatazwa sana na wazazi wetu kung’oa miti michanga, na wakati huo hatukuelewa kwamba wazee wetu walikuwa wanatufundisha utunzaji wa miti” akasema Balozi
Akielezea ni mikakati  gani ambayo serikali   kwa  kushirikiana na wadau mbalimbali inachuka katika  kukabiliana na  mabadiliko ya tabia nchi na  hiyo kuwa na uhakika wa usalama wa chakula, na  upatikanaji wa lishe bora.
Katibu Mkuu, ameeleza kwamba serikali  imejiwekea mipango  madhubuti ikiwamo ya  uhamasishaji wa wananchi  kuwa na matumizi bora na endelevu ya ardhi, misitu,  kilimo cha umwagiliaji pasi kutumia maji mengi na uhifadhi wa misitu.
Akasisitiza kwamba  mipango yote  iwe  ile inayoandaliwa na Umoja wa Mataifa Mashirika ya Kimataifa n ahata Serikali ili  tekelezeka na kuwa endelevu inapashwa kumilikiwa na wananchi ambao  hasa ndio waathirika wakubwa lakini pia  wanamchango mkubwa wa kuleta mabadiliko ili mradi wawezeshwe.
Akatahadharisha kwa kusema kama wananchi  hawatahusishwa  kwa  namna moja ama nyingine  basi utekelezaji wa  ajenda ya maendeleo endelevu  unaweza kuishia kwenye makabrasha.
Wanajopo wengine wakichangia katika  majadiliano hayo akiwamo Naibu Katibu Mkuu wa  Mapango wa Chakula Duniani, walieleza kwamba suala na usalama wa chakula na lishe linapashwa kupewa mkazo wa kipekee kwa kile walichosema, takwimu zinaonyea kwamba idadi kubwa na watu duniani wanathirika kwa ukosefu wa chakula lakini kubwa Zaidi  vyakula vyenye virutubisho na viini lishe.
Wakatoa mfano  kwa kusema kuwa wakati bei ya  vyakula aina ya nafaka ikushuka, bei ya   matunda na mboga mboga,  vyakula vitokanavyo na wanyama na  ambavyo ni muhimu katika ukuaji wa watoto chini ya miaka mitano vinazidi kupanda bei maradufu na wanaoathirika  ni watu maskini.
Na kwa sababu hiyo wakasisitiza kwamba kuna uwiano mkubwa kati ya mabadiliko ya  tabia nchi,  tatizo la usalama wa chakula na lishe duni mambo ambayo  serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali  zinatakiwa kushirikiana na  kuikabili changamoto hii ambayo athari zake ni kubwa.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...