WAZIRI
MKUU Mizengo Pinda(Pichani) amekabidhi magari mawili ya kubeba wagonjwa yenye thamani ya
sh. milioni 150 kwa uongozi wa Wilaya ya Ngorongoro ili yapelekwe kwenye kituo cha
afya cha Enduleni na hospitali ya Wasso ambayo inatumika kama hospitali ya wilaya.
Waziri
Mkuu amekabidhi magari hayo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa Septemba
2013 alipofanya ziara ya kikazi ya mkoa wa Arusha na kubaini adha ya usafiri
iliyokuwa ikiwapata wakazi wa kata za Wasso na Enduleni zilizoko wilayani
Ngorongoro.
Akizungumza
na watumishi wa idara ya afya na wananchi waliohudhuria makabidhiano hayo leo mchana,
(Jumanne, Septemba 8, 2015), Waziri Mkuu alisema aliyapata magari hayo kwa
wafadhili kutoka Japan na sehemu nyingine ambayo haikuitaja.
“Nikiwa
ziarani Japan, Machi mwaka huu, nilikutana na Watanzania waishio Japan nikawaomba
kama wanaweza kunisaidia gari la wagonjwa hata kama limetumika sababu najua
kule magari yaliyotumika huwa yanakuwa hayajachoka. Watanzania wale walikubali
na kuamua kunisaidia kutekeleza ahadi yangu,” alifafanua Waziri Mkuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...