WAZIRI MKUU Mizengo Pinda(Pichani) amekabidhi magari mawili ya kubeba wagonjwa yenye thamani ya sh. milioni 150 kwa uongozi wa Wilaya ya Ngorongoro ili yapelekwe kwenye kituo cha afya cha Enduleni na hospitali ya Wasso ambayo inatumika kama hospitali ya wilaya.

Waziri Mkuu amekabidhi magari hayo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa Septemba 2013 alipofanya ziara ya kikazi ya mkoa wa Arusha na kubaini adha ya usafiri iliyokuwa ikiwapata wakazi wa kata za Wasso na Enduleni zilizoko wilayani Ngorongoro.

Akizungumza na watumishi wa idara ya afya na wananchi waliohudhuria makabidhiano hayo leo mchana, (Jumanne, Septemba 8, 2015), Waziri Mkuu alisema aliyapata magari hayo kwa wafadhili kutoka Japan na sehemu nyingine ambayo haikuitaja.

“Nikiwa ziarani Japan, Machi mwaka huu, nilikutana na Watanzania waishio Japan nikawaomba kama wanaweza kunisaidia gari la wagonjwa hata kama limetumika sababu najua kule magari yaliyotumika huwa yanakuwa hayajachoka. Watanzania wale walikubali na kuamua kunisaidia kutekeleza ahadi yangu,” alifafanua Waziri Mkuu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...