Mtoto Baraka Dombeni, akiwa na mama yake Bizimana Violet,
akivishwa alama ya utambuzi muda mfupi baada ya kuwasili jana katika kambi ya
wakimbizi ya Nyarugusu, akitokea Wilaya ya Makamba nchini Burundi. Alama hii ni
utambulisho wa kuwawezesha wakimbizi wanaofika katika kambi ya Nyarugusu
kuandikishwa rasmi kabla ya kupewa hifadhi kambini hapo.
Afisa Msajili Msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la
kuwahudumia wakimbizi (UNHCR), Awadhi Nyanda akichukua taarifa toka kwa familia
mojawapo ya wakimbizi kutoka Burundi wanaoendelea kuingia nchini kuomba hifadhi. Wakimbizi hawa wanahifadhiwa katika kambi ya
Wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu Mkoani Kogoma.
Mkimbizi kutoka
Burundi, Sindaye Salvatory akiwa na wenzake, akiwekewa alama yake ya
utambulisho, wakati walipowasili katika Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu jana,
wakitokea nchini Burundi kuja kuomba hifadhi nchini Tanzania kutokana na hali
ya kisiasa nchini mwao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...