Mtoto Baraka Dombeni, akiwa na mama yake Bizimana Violet, akivishwa alama ya utambuzi muda mfupi baada ya kuwasili jana katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu, akitokea Wilaya ya Makamba nchini Burundi. Alama hii ni utambulisho wa kuwawezesha wakimbizi wanaofika katika kambi ya Nyarugusu kuandikishwa rasmi kabla ya kupewa hifadhi kambini hapo.
 Afisa Msajili Msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi (UNHCR), Awadhi Nyanda akichukua taarifa toka kwa familia mojawapo ya wakimbizi kutoka Burundi wanaoendelea kuingia nchini  kuomba hifadhi.  Wakimbizi hawa wanahifadhiwa katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu Mkoani Kogoma.
 Mkimbizi  kutoka Burundi, Sindaye Salvatory akiwa na wenzake, akiwekewa alama yake ya utambulisho, wakati walipowasili katika Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu jana, wakitokea nchini Burundi kuja kuomba hifadhi nchini Tanzania kutokana na hali ya kisiasa nchini mwao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...