Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Mstaafu, Francis Mutungi alisema kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 25 kuweka kipaumbele cha amani ambayo isiweze kuharibiwa kwa kutokana na uchaguzi.

Mtungi aliyasema hayo alipokutana na wahariri wa vyombo vya habari katika kusisitiza amani katika uchaguzi mkuu na kutaka waandishi kutumia kalamu vizuri kwani amani ikiharibika hakuna anayebaki salama.

Amesema matatizo ambayo yameanza kutokea katika kamapeni yanayotokana na mtu mmoja yasiwekwe katika sura ya taifa na kuonekana vyombo vya serikali vinashindwa kusimamia.

Jaji Mutungi amesema amani ikiangaliwa kwa jicho la karibu kwa kutambua kuna maisha baada  uchaguzi ambapo bila kufanya hivyo maisha hayatakuwepo.

“Waandishi kwa kutumia kalamu zenu mtafanya nchi ibaki kuwa na amani kwani wananchi wanaamini vyombo vya habari kwa kila hatua inayotokea katika uchaguzi mkuu”amesema Mutungi.

Aidha amesema amevitaka vyama vya siasa kutambua wajibu na sio kuangalia uchaguzi huru na haki kwani wajibu ndio utafanya vitu view salama na kuweza kuvuka suala hili la uchaguzi mkuu.
 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini,Jaji Mstaafu,Francis Mutungi akizungumza  mkutano wa wahariri na waandishi (hawapo pichani) juu ya amani kuelekea uchaguzi mkuu 25 ,uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
 Wahariri na waandishi wa habari wakimsikilia Msajili wa Vyama vya Siasa nchini,Jaji Mstaafu,Francis Murungi hayupo pichani katika mkutano wake uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Wahariri na waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na Msajili wa Vyama Siasa nchini,Jaji Mstaafu Francis Mutungi,jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...